LIGI KUU YA VODACOM KUENDELEA LEO
Ligi Kuu ya Vodacom inatarajiwa kuendelea kesho
kwa michezo sita kuchezwa katika viwanja
mbalimbali, ikiwa inaingia katika raundi ya tisa
huku kila timu ikisaka ushindi wa pointi tatu
muhimu.
Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Simba SC
watawakaribisha Coastal Union kutoka jijini
Tanga, mchezo utakaonza majira ya saa 10:30
jioni, huku Ndanda FC wakiwa wenyeji wa Stand
United uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini
Mtwara.
Wachimba Almasi wa Mwadui FC
watawakaribisha Yanga SC katika uwanja wa
Kambarage mjini Shinyanga, Toto African
watakua wenyeji wa maafande wa Mgambo
Shooting katika uwanja wa CCM Kirumba jijini
Mwanza.
Wakata miwa wa Turiani, Mtibwa Sugar watakua
wenyeji wa Kagera Sugar katika uwanja wa
Manungu Complex mkoani Morogoro, huku
watoza ushuru wa jiji la Mbeya katika uwanja wa
Sokoine Mbeya City watakua wenyeji wa Majimaji
kutoka mkoani Ruvuma.
Ligi hiyo itaendelea siku ya Alhamis kwa michezo
miwili kuchezwa, Tanzania Prisons watakua
wenyeji wa African Sports katika uwanja wa
Sokoine jijini Mbeya, JKT Ruvu watakua wenyeji
wa Azam FC katika uwanja wa Karume jijini Dar
es salaam.
Baraka Kizuguto
MEDIA & COMMUNICATION OFFICER
TFF
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous01 Oct 2016HII NDIO SIMBA NA YANGA, USIPITWE..
Ipo itikadi hata wengine huamini kwamba, utambulisho wa mtanzania ni alama ya chanjo ya mwili maaruf...
- Anonymous15 Apr 2016LIVERPOOL VS VILLARREAL NUSU FAINAL EUROPA
SHAKHTAR DONETSK vs SEVILLA VILLARREAL vs LIVERPOOL Droo ya Nusu Fainali ya Uefa Europa League imefa...
- Anonymous06 Apr 2016TFF KUWACHUKULIA HATUA KALI,VIONGOZI NA WATUMISHI WAKE
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesikitishwa na taarifa zilizosambaa katika m...
- Anonymous06 Apr 2016KUWAONA YANGA vs AL AHLY BUKU TANO TU...
Klabu ya Yanga, leo imetangaza viingilio vya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika dh...
- Anonymous30 Mar 2016WAAMUZI WA IVORY COAST KUWAAMUA YANGA
Waamuzi kutoka nchini Ivory Coast wamepewa jukumu la kuchezesha mechi kati ya Yanga dhidi ya Al Ahly...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni