Klabu ya Liverpool inakaribia kumteua meneja
wa zamani wa klabu ya Borussia Dortmund
Jurgen Klopp.
Majogoo hao wa jiji la Liverpool wanatarajiwa
kukamilisha makubaliano yao siku ya Alhamisi na
Klopp raia wa Ujerumani kuchukua rasmi mikoba
ya Brendan Rodgers mwishoni mwa juma hili,
kwa mkataba wa miaka mitatu.
Rodgers alitimuliwa siku ya Jumapili kufuatia
suluhu ya 1-1 dhidi ya Everton katika mchezo wa
ligi kuu ya England.
Klopp ameomba kuambatana na wasaidizi wake
wawili wa zamani katika benchi la ufundi ambao
ni Zeljko Buvac na Peter Krawietz.
Buvac raia wa Bosnia mwenye miaka 54 na
mjerumani Krawietz mwenye miaka 43, walitoa
ushirikiano mzuri na kupata mafanikio makubwa
wakifanya kazi pamoja klabuni Borussia
Dortmund.
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous01 Oct 2016HII NDIO SIMBA NA YANGA, USIPITWE..
Ipo itikadi hata wengine huamini kwamba, utambulisho wa mtanzania ni alama ya chanjo ya mwili maaruf...
- Anonymous15 Apr 2016LIVERPOOL VS VILLARREAL NUSU FAINAL EUROPA
SHAKHTAR DONETSK vs SEVILLA VILLARREAL vs LIVERPOOL Droo ya Nusu Fainali ya Uefa Europa League imefa...
- Anonymous06 Apr 2016TFF KUWACHUKULIA HATUA KALI,VIONGOZI NA WATUMISHI WAKE
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesikitishwa na taarifa zilizosambaa katika m...
- Anonymous06 Apr 2016KUWAONA YANGA vs AL AHLY BUKU TANO TU...
Klabu ya Yanga, leo imetangaza viingilio vya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika dh...
- Anonymous30 Mar 2016WAAMUZI WA IVORY COAST KUWAAMUA YANGA
Waamuzi kutoka nchini Ivory Coast wamepewa jukumu la kuchezesha mechi kati ya Yanga dhidi ya Al Ahly...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni