Mechi za raundi ya 11 za
Ligi Kuu Bara zilizokuwa
zichezwe Novemba 7 na 8
mwaka huu sasa zitafanyika
Desemba 12 na 13 kupisha
maandalizi ya Taifa Stars
ya mechi za mchujo za Kombe
la Dunia.
Taifa Stars inatarajia kuingia kambini
mapema mwezi ujao kujiandaa na mechi
ya kwanza dhidi ya Algeria ambayo
itafanyika Novemba 14 mwaka huu
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Timu hizo zitarudiana nchini Algeria,
Novemba 17 mwaka huu.
Mechi hizo za Vodacom
zitakazochezwa Desemba 12
ni kati ya Mgambo Shooting
na Yanga (Tanga), Kagera
Sugar na Ndanda (Tabora),
Stand United na Mwadui
(Shinyanga), Mbeya City na
Mtibwa Sugar (Mbeya), Azam
na Simba (Dar es Salaam) na
Majimaji na Toto Africans
(Songea). Mechi za Desemba
13 ni kati ya JKT Ruvu na
Tanzania Prisons (Dar es
Salaam), na Coastal Union
na African Sports (Tanga).
Pia mechi tatu za raundi ya
sita ambazo hazikuchezwa
Oktoba 4 mwaka huu kupisha
mechi ya Taifa Stars na
Malawi sasa zitafanyika
Desemba 16 mwaka huu. Mechi
hizo ni kati ya Azam na
Mtibwa Sugar (Dar es
Salaam), na African Sports
na Yanga (Tanga), mchezo
kati ya Ndanda na Simba
(Mtwara utapangiwa tarehe
ya kuchezwa.
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous01 Oct 2016HII NDIO SIMBA NA YANGA, USIPITWE..
Ipo itikadi hata wengine huamini kwamba, utambulisho wa mtanzania ni alama ya chanjo ya mwili maaruf...
- Anonymous15 Apr 2016LIVERPOOL VS VILLARREAL NUSU FAINAL EUROPA
SHAKHTAR DONETSK vs SEVILLA VILLARREAL vs LIVERPOOL Droo ya Nusu Fainali ya Uefa Europa League imefa...
- Anonymous06 Apr 2016TFF KUWACHUKULIA HATUA KALI,VIONGOZI NA WATUMISHI WAKE
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesikitishwa na taarifa zilizosambaa katika m...
- Anonymous06 Apr 2016KUWAONA YANGA vs AL AHLY BUKU TANO TU...
Klabu ya Yanga, leo imetangaza viingilio vya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika dh...
- Anonymous30 Mar 2016WAAMUZI WA IVORY COAST KUWAAMUA YANGA
Waamuzi kutoka nchini Ivory Coast wamepewa jukumu la kuchezesha mechi kati ya Yanga dhidi ya Al Ahly...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni