Mamlaka za uendeshaji Kesi huko Spain
zimeamua kumfutia Mashitaka Lionel Messi ya
ukwepaji Kodi.
Mamlaka hizo zimetoa uamuzi huo baada ya
kuafiki hoja kwamba wakati makosa hayo
yakitendeka Messi alikuwa na umri mdogo kiasi
cha kutojua nini kinaendelea.
Hata hivyo Kesi hiyo itaendelea kwa Baba yake
Messi aitwae Jorge Messi.
Messi, ambae ni Mchezaji wa Barcelona,
alishtakiwa yeye pamoja na Baba yake kwa
ukwepaji Kodi kati ya 2007 na 2009 unaokadiriwa
kufikia Euro Milioni 4.1.
Ukwepaji huo wa Kodi ni ule wa kuuza Haki za
Matangazo ya Staa huyo nje ya Spain na hivyo
kuikosesha Nchi hiyo mapato.
Licha ya kumfutia Mashitaka Messi, Waendesha
Mashitaka wa Kesi hiyo wamesema Messi
huenda akaitwa Mahakamani kutoa ushahidi dhidi
ya Baba yake ambae ndie Wakala wake tangu
aanze Soka.
Ikiwa atapatikana na hatia, Jorge Messi anaweza
kufungwa Miezi 18 au kupigwa Faini Euro Milioni
2 au vyote kwa pamoja.
Hata hivyo, mara baada ya tuhuma hizi kuibuka
Messi na Baba yake walilipa Kodi yote
waliyokuwa wakidaiwa pamoja na malimbikizo ya
Riba yake.
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous25 Nov 2016GERRARD HATA KAMA TUPO AFRIKA TUTAKUKUMBUKA DAIMA, KISOKA
Gwiji wa Liverpool, Steven Gerrard amestaafu rasmi kutumikia mchezo wa Soka ikiwa ni baada...
- Anonymous15 Jun 2016RATIBA LIGI KUU YA UINGEREZA 2016/17 HII HAPA
EPL August 13/14 Arsenal v Liverpool Bournemouth v Manchester United Burnley v Swa...
- Anonymous12 May 2016TIMU ZILIZOSHUKA DARAJA UINGEREZA HIZI HAPA
Klabu ya Norwich City imeshushwa daraja kutoka Ligi ya Premia licha ya kuandikisha ushindi dhidi ya ...
- Anonymous05 May 2016BOSI WA LEICESTER CITY AMWAGA MAGARI YA KIFAHARI KWA WWCHEZAJI
Mercedes B-Class Electric Drive. Thamani yake ni pauni £32,670 (zaidi ya Sh million 103) kwa g...
- Anonymous06 Apr 2016UEFA CHAMPIONZ LIGI ROBO FAINALI
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku Jumatano Aprili 6 Paris St-Germain v Manchester City ...
- Anonymous29 Mar 2016MOURINHO KUIJENGA UNITED
Meneja wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho anadaiwa kuanza kujipanga na Manchester United kama atac...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni