Licha ya kupanda nafasi nne hadi nambari
136,Tanzania imeorodheshwa ya chini zaidi na
shirikisho la soka duniani FIFA katika soka ya
Afrika mashariki.
Kulingana na orodha ya FIFA iliotolewa siku ya
Alhamisi,Uganda imeorodheshwa ya 75,ikifuatiwa
na Rwanda katika nafasi ya 93.
Uganda na Rwanda zimeshuka nafasi 4 na 15
mtawalia.
Burundi nayo imerodheshwa nambari ya 113
ikiwa ya tatu ikifuatiwa na Kenya katika nafasi ya
131 ikiwa nambari 4.
Taifa Stars ya Tanzania ambayo ililazimu sare ya
0-0 dhidi ya timu ya Super Eagles kutoka Nigeria
katika mechi za kufuzu kwa kombe la Afrika
inashikila nafasi ya 5 na ya mwisho katika Afrika
mashariki ikiwa katika nambari 136 duniani.
Kwengineko orodha hiyo mpya inaonyesha kuwa
Liberia na Afrika Kusini ndizo zilizofanywa vyema.
Mataifa hayo mawili yameorodheshwa ya 95
baada ya kupanda kwa nafasi 65 na 144 baada
ya kupanda kwa nafasi 54 mtawalia.
Kulingana na Shrikisho la FIFA,Ujerumani
inaongoza ikifuatiwa na Argentina kisha Ubelgiji
nafasi ya 3 na Ureno katika nafasi ya nne.
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous01 Oct 2016HII NDIO SIMBA NA YANGA, USIPITWE..
Ipo itikadi hata wengine huamini kwamba, utambulisho wa mtanzania ni alama ya chanjo ya mwili maaruf...
- Anonymous15 Apr 2016LIVERPOOL VS VILLARREAL NUSU FAINAL EUROPA
SHAKHTAR DONETSK vs SEVILLA VILLARREAL vs LIVERPOOL Droo ya Nusu Fainali ya Uefa Europa League imefa...
- Anonymous06 Apr 2016TFF KUWACHUKULIA HATUA KALI,VIONGOZI NA WATUMISHI WAKE
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesikitishwa na taarifa zilizosambaa katika m...
- Anonymous06 Apr 2016KUWAONA YANGA vs AL AHLY BUKU TANO TU...
Klabu ya Yanga, leo imetangaza viingilio vya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika dh...
- Anonymous30 Mar 2016WAAMUZI WA IVORY COAST KUWAAMUA YANGA
Waamuzi kutoka nchini Ivory Coast wamepewa jukumu la kuchezesha mechi kati ya Yanga dhidi ya Al Ahly...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni