Mazembe Imetisha africa, kufuatia mshambuliaji Mbwana Ally
Samata kufunga mabao mawili katika ushindi
wa 3-0 dhidi ya El Merreikh ya Sudan.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Tanzania,
amefunga mabao hayo katika mchezo wa
marudiano wa Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa
Afrika na kuiwezesha TP Mazembe kwenda
fainali ya michuano hiyo kwa mara ya kwanza
baada ya miaka mitano.
Nyota wa zamani wa Simba SC ya Dar es
Salaam, Samatta alifunga bao la kwanza dakika
ya 53, akimalizia pasi ya Adama Traore kabla
ya kufunga la pili dakika ya 69 kwa pasi ya Yaw
Frimpong.
Mshambuliaji mwingine wa Tanzania, Thomas
Emmanuel Ulimwengu aliyeingia kipindi cha pili
kuchukua nafasi ya Rainford Kalaba alishiriki
bao la tatu lililofungwa na Roger Assale dakika
ya 71.
Mazembe inayosonga mbele kwa ushindi wa
jumla wa 4-2 baada ya awali kufungwa 2-1
Khartoum, sasa itakutana na USM Alger iliyoitoa
El HIlal ya Sudan katika fainali ya Ligi ya
Mabingwa AFrika mwaka huu.
Kikosi cha Mazembe kilikuwa; R. Kidiaba/T.
Ulimwengu dk58, J. Kasusula, Y. Frimpong, J.
Kimwaki, S. Coulibaly, Asante/R. Assale dk46,
B. Diarra, D. Adjei Nii/ M. Bokadi dk85, R.
Kalaba, M. Samatta na A. Traore.
El Merreikh; J. Salim, Ala'a Eldin Yousif, Musaab
Omer, Ayman Saied, Ragei Abdallah, Amir
Kamal, Ramadan Agab, D. Libere/Ahmed Abdalla
dk68, Bakri Al Madina, S. Jabason na F. Coffie/
Omar Bakheet dk69.
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous25 Nov 2016GERRARD HATA KAMA TUPO AFRIKA TUTAKUKUMBUKA DAIMA, KISOKA
Gwiji wa Liverpool, Steven Gerrard amestaafu rasmi kutumikia mchezo wa Soka ikiwa ni baada...
- Anonymous15 Jun 2016RATIBA LIGI KUU YA UINGEREZA 2016/17 HII HAPA
EPL August 13/14 Arsenal v Liverpool Bournemouth v Manchester United Burnley v Swa...
- Anonymous12 May 2016TIMU ZILIZOSHUKA DARAJA UINGEREZA HIZI HAPA
Klabu ya Norwich City imeshushwa daraja kutoka Ligi ya Premia licha ya kuandikisha ushindi dhidi ya ...
- Anonymous05 May 2016BOSI WA LEICESTER CITY AMWAGA MAGARI YA KIFAHARI KWA WWCHEZAJI
Mercedes B-Class Electric Drive. Thamani yake ni pauni £32,670 (zaidi ya Sh million 103) kwa g...
- Anonymous06 Apr 2016UEFA CHAMPIONZ LIGI ROBO FAINALI
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku Jumatano Aprili 6 Paris St-Germain v Manchester City ...
- Anonymous29 Mar 2016MOURINHO KUIJENGA UNITED
Meneja wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho anadaiwa kuanza kujipanga na Manchester United kama atac...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni