TAYARI Nafasi 3 kati ya 16 za Raundi ya Mtoano ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL, zimeshachukuliwa na Klabu 3 na bado zipo Klabu 27 kati ya 29 zilizobaki kwenye Makundi zenye nafasi za kuchukua Nafasi 13 zilizobaki.
KLABU ZILIZOFUZU KUINGIA MTOANO:
-Real Madrid
-Manchester City
-Zenit Saint Petersburg
IFUATAYO NI HALI YA KILA KUNDI KWA MECHI ZA JUMANNE NA JUMATANO:
Jumanne Novemba 24
KUNDI E:
-Barcelona (Pointi 10) v Roma (5)
-BATE Borisov (3) v Bayer Leverkusen (4)
Barcelona watasonga kama Washindi wa Kundi wakipata Sare na pia wanaweza kufuzu wakifungwa ikiwa Leverkusen watashindwa kushinda.
Ikiwa BATE na Leverkusen zitatoka Sare basi watupwa nje ya Timu mbili za juu ikiwa AS Roma watashinda.
Ikiwa BATE watafungwa na AS Roma kushinda, BATE watamaliza Nafasi ya 4.
KUNDI F:
-Bayern München (Pointi 9) v Olympiacos (9)
-Arsenal (3) v Dinamo Zagreb (3)
Sare kwa Bayern na Olympiacos itawatosha kutinga Raundi ya Mtoano.
Arsenal wanahitaji kushinda na kuombea Olympiacos wafungwe ili wapate nafasi ya kuifunga Olympiacos katika Mechi ya mwisho ya Kundi na wao kufuzu lakini inabidi ushindi uwe bora kuliko Olympiacos walipoifunga Arsenal 3-2 katika Mechi yao ya kwanza.
Arsenal hawawezi kuipita Bayern.
KUNDI G:
-Porto (Pointi 10) v Dynamo Kyiv (5)
-Maccabi Tel-Aviv (0) v Chelsea (7)
Porto watafuzu kwa Sare.
Chelsea watafuzu wakishinda na Dynamo kushindwa kupata ushindi.
KUNDI H:
-Zenit (Pointi 12, Washafuzu) v Valencia (6)
-Lyon (1) v Gent (4)
Zenit wameshafuzu na watatwaa Nafasi ya Kwanza ya Kundi wakishinda.
Valencia watafuzu wakishinda huku Gent wasishinde.
Jumatano Novemba 25
KUNDI A :
-Malmö (Pointi 3) v Paris Saint-Germain (7)
-Shakhtar Donetsk (3) v Real Madrid (10, Washafuzu)
Real Madrid wameshafuzu na watashinda Kundi hili wakiwa Namba 1 ikiwa watashinda au wakitoka Sare ikiwa PSG haishindi n ahata wakifungwa wanaweza kuwa Namba 1 ikiwa PSG itafungwa.
PSG watafuzu wakishinda au kwa Sare ikiwa Shakhtar haishindi.
KUNDI B:
-CSKA Moskva (Pointi 4) v Wolfsburg (6)
-Manchester United (7) v PSV Eindhoven (6)
Man United watafuzu wakishinda.
CSKA hawatafuzu wakifungwa.
KUNDI C:
-Astana (Pointi 3) v Benfica (9)
-Atlético Madrid (8) v Galatasaray (4)
Benfica watasonga wakishinda na pia wakitoka Sare ikiwa Atletico itaifunga Galatasaray au kwenda Sare.
Ikiwa Benfica watashinda na Atletico hawashindi, basi Benfica watatwaa Nafasi ya Kwanza.
Atlético wanahitaji Sare kufuzu.
KUNDI D:
-Juventus (Pointi 8) v Manchester City (9, Washafuzu)
-Borussia Mönchengladbach (2) v Sevilla (3)
Man City wameshafuzu na watatwaa Nafasi ya Kwanza kwa ushindi.
Juventus watafuzu wakishinda au wakipata matokeo yeyote yale ili mradi Sevilla wasishinde.
Ili kuweka hai matumaini ya kufuzu, Sevilla lazima waifunge Mönchengladbach na kungojea Mechi ya mwisho na Juventus hapo Desemba 8 washinde ili wafuzu ingawa kwenye Mechi hiyo wasipoifunga Juve basi wabahakika ya kwenda EUROPA LIGI ambako walitwaa Ubingwa wake kwa Misimu Miwili iliyopita.
UEFA CHAMPIONZ LIGI
RATIBA
**Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku, isipokuwa inapotajwa
Jumanne Novemba 24
KUNDI E
2000 BATE Borislov v Bayer Leverkusen
Barcelona v AS Roma
KUNDI F
Arsenal v Dinamo Zagreb
Bayern Munich v Olympiakos
KUNDI G
FC Porto v Dynamo Kiev
Maccabi Tel Aviv v Chelsea
KUNDI H
2000 Zenit Saint Petersburg v Valencia
Lyon v KAA Gent
Jumatano Novemba 25
KUNDI A
Malmö FF v Paris St Germaine
Shakhtar Donetsk v Real Madrid
KUNDI B
2000 CSKA v VfL Wolfsburg
Man United v PSV Eindhoven
KUNDI C
1800 FC Astana v Benfica
Atletico Madrid v Galatasaray
KUNDI D
Borussia Mönchengladbach v Sevilla
Juventus v Man City
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous25 Nov 2016GERRARD HATA KAMA TUPO AFRIKA TUTAKUKUMBUKA DAIMA, KISOKA
Gwiji wa Liverpool, Steven Gerrard amestaafu rasmi kutumikia mchezo wa Soka ikiwa ni baada...
- Anonymous15 Jun 2016RATIBA LIGI KUU YA UINGEREZA 2016/17 HII HAPA
EPL August 13/14 Arsenal v Liverpool Bournemouth v Manchester United Burnley v Swa...
- Anonymous12 May 2016TIMU ZILIZOSHUKA DARAJA UINGEREZA HIZI HAPA
Klabu ya Norwich City imeshushwa daraja kutoka Ligi ya Premia licha ya kuandikisha ushindi dhidi ya ...
- Anonymous05 May 2016BOSI WA LEICESTER CITY AMWAGA MAGARI YA KIFAHARI KWA WWCHEZAJI
Mercedes B-Class Electric Drive. Thamani yake ni pauni £32,670 (zaidi ya Sh million 103) kwa g...
- Anonymous06 Apr 2016UEFA CHAMPIONZ LIGI ROBO FAINALI
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku Jumatano Aprili 6 Paris St-Germain v Manchester City ...
- Anonymous29 Mar 2016MOURINHO KUIJENGA UNITED
Meneja wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho anadaiwa kuanza kujipanga na Manchester United kama atac...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni