Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Na Sophia Mwaipyana,Chunya
 
Mdau wa michezo wilayani Chunya mkoani Mbeya Reonad Manyesha amejitolea kujenga  moja ya viwanja ambavyo vinatakiwa kujengwa ndani ya uwanja wa kisasa unaotalajiwa kujegwa katika kata ya Mbugani wilayani humo.
 
Uwanja huo ambao unajengwa na halimashauli ya wilaya ya chunya  kwasasa wako katika hatua ya awali ya kufyatua matofari na unatarajiwa kuwa na viwanja vyote vya michezo ndani ya uwanja huo.
 
 
 
Akiongea na Championi Ijuma Manyesha amesema kuwa yeye kajitolea kujenga uwanja wa mpira wa wavu ambao utaghalimu shilingi milioni ishirini na tano na utachukuwa mada wa miezi sita.
 
“Lengo langu kubwa ni kumuunga mkono mkuu wa wilaya yetu katika ujenzi wauwanja huu wakisasa ambao tunatalajia kujenga katika kata yetu ya Mbugani kwahiyo mimi kama mzawa wa hapa niliona vyema kujitoa kwasababu uwanja huu niwetu sisi wanachunya nasiyo wamkuu wa wilaya”
 
“Iwapo uwanja huu wakisasa utakamilika hapa wilayani kwetu tuta ongeza ajira kwa vijana wetu kupitia michezo  na tutachangia katika maendeleo ya wilaya yetu hivyo mji wa chunya utakuwa kwakasi”
 
“Nawaomba wadau wengine wajitokeze kujitolea kujenga uwanja huu siyo wakazi wa chunya peke niwadau wote wamkoa wa Mbeya tunaomba watusapoti kwani haya nimaendeleo ya mkoa wetu”
 
“Rameck Kwawilo mmoja wa wadau wa michezo wilayani humo alisema kuwa wanampongeza Manyesha kwa kujitoa kuendeleza michezo katika wilaya hiyo kwa kujenga uwanja”
 
“Naimani hata  watu wengine pia wataiga mfano kutoka kwa mwenzetu alivyo fanya siyo lazima utoe pesa hata kuja kusaidia shughuli ndogondogo zina zoendelea kwasasa  unakuwa umesaidia kwahiyo matajili waliopo chunya wajitoe kama Manyesha”.
 
Mwisho


Chapisha Maoni