KEPTENI wa Manchester United Wayne Rooney
ameruhusiwa kufanyiwa Mechi ya Kumuenzi na
mapato yote ya Mechi hiyo kwenda kwenye
Mifuko ya Hisani.
Mechi hii imepitishwa baada ya Mashabiki
kuiomba Klabu kutambua mchango mkubwa
uliotukuka wa Rooney kwa Klabu hiyo.
Sasa Mechi hii itachezwa Old Trafford hao Agosti
3, 2016 dhidi ya Wapinzani ambao watapangwa
baadae.
Akiongelea uamuzi huu, Rooney alisema: “Usiku
wa Mechi utakuwa spesho kwangu na Familia
yangu na nategemea tunaweza pia tukaleta kitu
kimoja au viwili vya kushtukiza!”
Nae Mtendaji Mkuu wa Man United, Ed Woodward
amesema: "Kuanzia Mechi yake ya kwanza
aliyopiga Hetitriki hadi sasa ana Goli 236, Wayne
amekuwa ndio Mtu mkuu
Katika kipindi cha mafanikio makuu ya Klabu!”
Habari hizi zimekuja wakati Oktoba 24 Rooney
alitimiza Umri wa Miaka 30 na katika kipindi
ambacho ananyooshewa kidole kuhusu uchezaji
wake akiwa amefunga Bao 2 tu za Ligi katika
Mechi 9 Msimu huu.
Rooney, ambae alihamia Man United Mwaka 2004
akitoka Everton, ndie Mfungaji Bora wa 3 katika
Man United akiwa nyuma ya Sir Bobby Charlton,
Bao 249, na Denis Law, Bao 237, akiwa 1 tu
mbele ya Rooney.
Mafanikio mengine ya Rooney akiwa na Man
United ni kutwaa Ubingwa wa England mara 5 na
UEFA CHAMPIONZ LIGI mara 1.
Pia amebakisha Mechi 7 tu kuwa Mchezaji wa 10
kwa Man United kufikisha Mechi 500.
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous25 Nov 2016GERRARD HATA KAMA TUPO AFRIKA TUTAKUKUMBUKA DAIMA, KISOKA
Gwiji wa Liverpool, Steven Gerrard amestaafu rasmi kutumikia mchezo wa Soka ikiwa ni baada...
- Anonymous15 Jun 2016RATIBA LIGI KUU YA UINGEREZA 2016/17 HII HAPA
EPL August 13/14 Arsenal v Liverpool Bournemouth v Manchester United Burnley v Swa...
- Anonymous12 May 2016TIMU ZILIZOSHUKA DARAJA UINGEREZA HIZI HAPA
Klabu ya Norwich City imeshushwa daraja kutoka Ligi ya Premia licha ya kuandikisha ushindi dhidi ya ...
- Anonymous05 May 2016BOSI WA LEICESTER CITY AMWAGA MAGARI YA KIFAHARI KWA WWCHEZAJI
Mercedes B-Class Electric Drive. Thamani yake ni pauni £32,670 (zaidi ya Sh million 103) kwa g...
- Anonymous06 Apr 2016UEFA CHAMPIONZ LIGI ROBO FAINALI
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku Jumatano Aprili 6 Paris St-Germain v Manchester City ...
- Anonymous29 Mar 2016MOURINHO KUIJENGA UNITED
Meneja wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho anadaiwa kuanza kujipanga na Manchester United kama atac...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni