Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Mwaka 1994 wachezaji wakubwa wa Yanga wa kitanzania waliingia kwenye mgogoro wa Yanga asili na Yanga kampuni na kuamua kuukomoa uongozi wa timu.
 Walifungwa na Simba 4-1 kwa kinachosadikiwa kutekeleza mgomo huo. Yanga hii ilikuwa ya kina makipa Steven Nemes na Rifat Said,mabeki Ngandou Ramadhan, Joseph Lazaro, Kenneth Mkapa, Willy Mtendamema, Costantine Kimanda na Willy Martin.
Viungo wa kati walikuwa Method Mogella, Mwanamtwa Kihwelo, Said Mwamba, Sekilojo Chambua na wa pembeni (mawinga) David Mjanja, Sanifu Lazaro na Edibily Lunyamila.
Wafunga mabao walikuwa Mohammed Hussein Mmachinga, James Tungaraza na Ally Yussuf “Tigana” miongoni mwa wachezaji wengine.
Mgogoro huo ulisababisha kipa Rifat Said kurudi Zanzibar, Edibily Lunyamila kuchukuliwa na Malindi ya Zanzibar kwa msimu mmoja, Steven Nemes na Said Mwamba kujiunga na Simba baada ya mgogoro huo kuwa mkubwa huku kocha Tambwe Leya akikisuka kikosi cha watoto wenye kipaji cha soka aliowakusanya. Alikiita kikosi hicho cha watoto Black Stars.

Miongoni mwa wachezaji wa kikosi hicho walikuwa Anwar Awadh, Mzee Abdallah, Silvatus Ibrahim “Polisi”, Maalim Saleh “Romario”, Nonda Shaaban “Papii” na wengine. Tukumbushane kwamba katika kipindi hicho, tangu kipigo cha 4-1 toka kwa Simba. Yanga ilikuwa ikifungwa mfululizo na Simba na mwiba wao mkali ulikuwa Madaraka Selemani, Mzee wa Kiminyio.
Baada ya vijana wengi wa Black Stars kujumuishwa kwenye kikosi cha kwanza cha Yanga, likaja pambano la Yanga na Simba na Madaraka akiwemo. Pambano hilo la kwanza msimu wa 1996, lilimalizika kwa suluhu huku Mzee wa Kiminyio akiminywa vilivyo na kijana mdogo Anwar Awadh aliyekuwa beki wa kushoto. Baada ya mechi, mashabiki wa Yanga walimbeba juu juu Anwar kwani hawakuamini kama angeweza kumzuia hivyo Madaraka.
Baadhi ya vijana hawa walikuja kuijenga Yanga imara iliyokuja kucheza ligi ya kwanza ya nane bora ya ubingwa wa Afrika mwaka 1998 na kubeba ubingwa wa Afrika mashariki na ya kati nchini Uganda mwaka 1999 huku ikitoa mchezaji mkubwa wa dunia, Nonda Shaaban.
Lakini iliwai tokea kwa upande wa simba
Simba walinibebesha Gunia la Misumari.
 Mbuyi yondani
“Mwaka 1993 wakati nikiwa Simba,nilikosa bao la wazi wakati zikiwa zimesalia dakika 3 mpira kumalizika,katika kombe la Caf kwa sasa shirikisho,kati ya Simba na Timu Toka Msumbiji,nakumbuka ilikuwa CCM Kirumba Mwanza mchezo ambao ulimalizika kwa sare ya bila kufungana.



“Baada ya mechi ile sikuwa na amani,wenye timu walinitazana kwa jicho baya  huku wakinituhumu kuwa mimi ni mpenzi wa Yanga na kwamakusudi nikaamua kuwakosesha Simba ushindi kiukweli iliniuma sana.


“Basi kutokana na tuuma ile na licha ya kwamba kiwango changu kilikuwa kikubwa masikini ya mungu sikupewa nafasi hata ya kusafiri na timu kwenda nchini Msumbiji katika mechi ya marudiano waliniacha Bongo.

“Kuanzi hapo nilichukiwa sana hadi nikahasirika kisaikorojia pindi nikiwapo uwanjani lakini ukweli ni kwamba mimi sikuwa na mapenzi na Yanga na kukosa Bao ni suala la kawaidi kwa mchezaji sio makusudi.


Chapisha Maoni