Kakaake mkubwa nyota wa timu ya Argentina na
Barcelona Lionel Messi amekamatwa kwa
kumiliki bunduki bila kibali.
Matias Messi alisimamishwa na maafisa wa
polisi wakati wa ukaguzi siku ya jumapili.
Polisi wanasema kuwa Matias mwenye umri wa
miaka 33 alikataa kuonyesha vibali vyake
aliposimamishwa katika mji wa Rosario.
Polisi walilikagua gari lake na kupata bunduki
ambayo Matias ameshindwa kutoa kibali chake
cha umiliki.
Maafisa hao wanasema kulikuwa na mvutano kati
yao na ndugu huyo wa Messi ,ambapo alijeruhiwa
katika jicho huku maafisa hao wakipata majeraha
madogo.
Baadaye alipelekwa katika kituo kimoja cha polisi
mjini Rosario na kuzuiliwa kwa kwa saa nne.
Alikamatwa mara moja kabla ya mwaka 2008
kwa kubeba silaha bila kibali.
Watu wa familia ya Messi pia wanakabiliwa na
madai ya kukwepa kulipa kodi nchini Uhispania.
Lionel Messi na babaake Jorge wote
wanatuhumiwa kuiibia mamlaka zaidi ya yuro
milioni 4 zinazohusishwa na mapato kutokana na
matumizi ya jina lake.
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous25 Nov 2016GERRARD HATA KAMA TUPO AFRIKA TUTAKUKUMBUKA DAIMA, KISOKA
Gwiji wa Liverpool, Steven Gerrard amestaafu rasmi kutumikia mchezo wa Soka ikiwa ni baada...
- Anonymous15 Jun 2016RATIBA LIGI KUU YA UINGEREZA 2016/17 HII HAPA
EPL August 13/14 Arsenal v Liverpool Bournemouth v Manchester United Burnley v Swa...
- Anonymous12 May 2016TIMU ZILIZOSHUKA DARAJA UINGEREZA HIZI HAPA
Klabu ya Norwich City imeshushwa daraja kutoka Ligi ya Premia licha ya kuandikisha ushindi dhidi ya ...
- Anonymous05 May 2016BOSI WA LEICESTER CITY AMWAGA MAGARI YA KIFAHARI KWA WWCHEZAJI
Mercedes B-Class Electric Drive. Thamani yake ni pauni £32,670 (zaidi ya Sh million 103) kwa g...
- Anonymous06 Apr 2016UEFA CHAMPIONZ LIGI ROBO FAINALI
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku Jumatano Aprili 6 Paris St-Germain v Manchester City ...
- Anonymous29 Mar 2016MOURINHO KUIJENGA UNITED
Meneja wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho anadaiwa kuanza kujipanga na Manchester United kama atac...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni