Hatimaye Kocha Charles
Boniface Mkwasa amesaini
mkataba wa mwaka mmoja
kuinoa Taifa Stars.
Mkwasa amesaini mkataba wa
kuinoa Stars ambao utaisha
Machi 31, mwaka huu.
"Kweli nimsaini mkataba,
nawashukuru sana TFF kwa
kuniamini na kunipa jukumu
hili," alisema.
Mkwasa ambaye mkataba wake
na Yanga uliokuwa unaisha
Desemba mwaka huu, amesema
amepanga kuwaanga Yanga
rasmi.
Kocha huyo tayari
ameiongoza Stars kucheza
mechi mbili za mashindano
akiwa kocha wa muda na
aliiwezesha kutoka sare ya
1-1 dhidi ya Uganda katika
michuano ya Chan.
Mechi ya pili, Mkwasa
aliiongoza Taifa Stars
kutoka sare ya bila kufunga
dhidi ya Nigeria katika
mechi ya kuwania kucheza
Afcon.
Sasa kesho atakuwa na
kibarua cha tatu dhidi ya
Malawi kwenye Uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam
na kitakuwa cha kwanza
kwake akiwa kocha kamili wa
Taifa Stars.
Mkwasa ameichukua Stars
baada ya Mholanzi, Mart
Nooij kushinda na kuifanya
iwe sawa na jahazi
linaloyumba.
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous01 Oct 2016HII NDIO SIMBA NA YANGA, USIPITWE..
Ipo itikadi hata wengine huamini kwamba, utambulisho wa mtanzania ni alama ya chanjo ya mwili maaruf...
- Anonymous15 Apr 2016LIVERPOOL VS VILLARREAL NUSU FAINAL EUROPA
SHAKHTAR DONETSK vs SEVILLA VILLARREAL vs LIVERPOOL Droo ya Nusu Fainali ya Uefa Europa League imefa...
- Anonymous06 Apr 2016TFF KUWACHUKULIA HATUA KALI,VIONGOZI NA WATUMISHI WAKE
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesikitishwa na taarifa zilizosambaa katika m...
- Anonymous06 Apr 2016KUWAONA YANGA vs AL AHLY BUKU TANO TU...
Klabu ya Yanga, leo imetangaza viingilio vya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika dh...
- Anonymous30 Mar 2016WAAMUZI WA IVORY COAST KUWAAMUA YANGA
Waamuzi kutoka nchini Ivory Coast wamepewa jukumu la kuchezesha mechi kati ya Yanga dhidi ya Al Ahly...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni