Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Meneja wa Chelsea Jose Mourinho amefunguliwa
mashitaka na FA, Chama cha Soka England, kwa
utovu wa nidhamu.
Maneno ambayo yanaweza kumsulubu Mourinho
yalitolewa Jumamosi mara baada ya Chelsea
kuchapwa 3-1 na Southampton kwenye Mechi ya
Ligi Kuu England iliyochezwa Uwanjani Stamford
Bridge.
FA imedai maneno ya Mourinho yanamaanisha
Marefa wanapendelea na hivyo ni kinyume cha
Sheria.
Kwenye Mechi hiyo na Southampton Mourinho
alichukizwa na Refa Robert Madley kuwanyima
Penati na kudai Marefa huogopa kuwapa Chelsea
Penati.
Mourinho, mwenye Miaka 52, amepewa hadi
Alhamisi Oktoba 8 Saa 2 Usiku kwa Saa za
Tanzania, kujibu mashitaka hayo.
Hiyo Jumamosi, mara baada ya kutoa kauli yake,
Mourinho pia alitabiri FA itamfungulia mashitaka.
Licha ya kusakamwa na vipigo Vinne katika
Mechi 8 za Ligi Kuu England ambayo wao ndio
Mabingwa na kutupwa Nafasi ya 16 wakiwa
Pointi 10 nyuma ya Vinara Man City, Klabu ya
Chelsea Jana ilisema bado wana imani na
Mourinho.



Chapisha Maoni