Kikosi cha timu ya Taifa ya
Tanzania (Taifa Stars)
inayodhaminiwa na bia ya
Kilimanjaro Premium Lager
kimeanza mazoezi leo mchana
katika uwanja wa Taifa
kujiandaa na mchezo dhdi ya
Malawi utakaocheza Jumatano
Oktoba 7, 2015 kuwania
kufuzu kwa Fainali za Kombe
la Dunia mwaka 2018 nchini
Urusi.
Stars inayonolewa na kocha
mkuu mzawa Charles Mkwasa,
akisaidiwa na Hemed
Morroco, Peter Manyika na
mshauri wa Ufundi Abdallah
Kibadeni wameingia kambini
jana katika hoteli ya Urban
Rose iliyopo Kisutu jijini
Dar es Salaam.
Wachezaji wote wameripoti
kambini isipokuwa wachezaji
wa kimataifa wanaocheza
soka la kulipwa nje ya
nchi, Mrisho Ngasa, Mbwana
Samata na Thomas Ulimwengu
wanaotarajiwa kuungana na
wenzao mwishoni mwa wiki
baada ya kumaliza michezo
inayowakabili wikiendi hii.
Wachezaji waliopo kambini
ni magolikipa All Mustafa,
Aishi Manula, Said Mohamed,
walinzi Juma Abdul, Shomari
Kapombe, Mohamed Hussein,
Haji Mwinyi, Hassan
Isihaka, Kelvin Yondani na
nahodha Nadir Haroub
“Cannavaro”.
Wengine ni viungo Himid
Mao, Mudathir Yahya, Frank
Domayo, Said Ndemla, Salum
Telela, Deus Kaseke, Saimon
Msuva, Farid Musa,
washambuliaji John Bocco,
Rashid Mandawa na Ibrahim
Hajibu
Asante kwa kutembelea Hope FM Iringa, Asante kwaku-share habari hii, Kama una Maoni, Ushauri, Story ya ku-share na sisi na au Unahitaji msaada...!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Wasiliana nasi kwa Email hopefmiringa@gmail.com au ungana nasi kupitia mitandao ya kijamii hapo chini!
Related Posts
- Anonymous01 Oct 2016HII NDIO SIMBA NA YANGA, USIPITWE..
Ipo itikadi hata wengine huamini kwamba, utambulisho wa mtanzania ni alama ya chanjo ya mwili maaruf...
- Anonymous15 Apr 2016LIVERPOOL VS VILLARREAL NUSU FAINAL EUROPA
SHAKHTAR DONETSK vs SEVILLA VILLARREAL vs LIVERPOOL Droo ya Nusu Fainali ya Uefa Europa League imefa...
- Anonymous06 Apr 2016TFF KUWACHUKULIA HATUA KALI,VIONGOZI NA WATUMISHI WAKE
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesikitishwa na taarifa zilizosambaa katika m...
- Anonymous06 Apr 2016KUWAONA YANGA vs AL AHLY BUKU TANO TU...
Klabu ya Yanga, leo imetangaza viingilio vya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika dh...
- Anonymous30 Mar 2016WAAMUZI WA IVORY COAST KUWAAMUA YANGA
Waamuzi kutoka nchini Ivory Coast wamepewa jukumu la kuchezesha mechi kati ya Yanga dhidi ya Al Ahly...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni