Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Hamis  Mtepa
TAREHE31-03-2014.




Displaying IMG_0291.jpg







               Katika orodha  ya wachezaji mahili waliowai tokea katika nafasi ya goli kipa kwa  soka la hapa nchini  Hamis mtepa  ni miongoni mwao, ambaye aliwika akiwa na Tenesco ya songea pamoja na Maji Maji  na kujizolea umaarufu mkubwa  kwa uwezo wake mkubwa wa kurinda lango.

Mtepa mzaliwa wa Mtwara huku Mnazi Mmoja[Lindu] alianza kusakata kandanda katika shule ya msingi songea zamani ikifahamika kwa jina la majengo ambapo nyota yake ilizidi kung’aa Zaidi alipojiunga na timu ya mtaani ya Olimbiki Rangers mwaka 1984 wakati bado akiwa mdogo.

Baada ya kuitimu elimu ya shule ya msingi mtepa alijiunga na masomo ya sekondari katika shule ya luwiko songea mjini lakini kwa bahati mbaya alikatisha masomo kwa matatizo ya kifamilia ambapo  akatimkia Mtwara, akiwa huko alikiputa na timu ya ushirika ya  mtwara timu ambayo akuchezea kwa muda mrefu akasajiliwa na timu ya kiwanda cha misitu mafinga ambako aliitumikia kwa msimu mmoja na mnamo mwaka 1988 alitua Tanesco ya songea hapo ndipo kipaji chake kilionekana baada ya kufanikiwa kuipandisha timu hiyo toka ligi daraja la Tatu adi ligi kuu kipindi kile ligi daraja la kwanza.

Mwaka 1993 kwa mara ya kwanza alicheza mechi chache za ligi kuuu akiwa na Tanesco lakini baadae  ilitokea stofahamu ambapo Mkurugenzi wa Tanesco Simon Mwavile aliwasimamisha wachezaji wote wa Tanesco kucheza mpira na akawapa onjo kali na kuwaambia asiyetaka kufanya kazi Tanesco akacheze mpira, basi timu ikavurugika na ukawa mwisho wa kucheza ligi kuu.

Baada ya seke seke hilo yeye,Amburosi pamoja na Mbopa Luoga walisajiliwa na timu ya Soka ya Maji Maji,kipindi hicho Wanalizombe walikuwa na kipa Shaibu Kambanga  pekee ambapo walikuwa wakimwitaji sana Mtepa kutokana na umahili wake wa kuringa lango lakini kitu ambacho kilitokea baada ya kucheza mechi mbili za nyumbani Tanesco walimzuia kusafiri na Maji Maji na wakamwamishia  Mtwara kikazi ili kumkomesha.

Akiwa Mtwara mwaka 1994 Tanesco walimruhusu kuchezea Taifa cup akiwa na timu ya Mkoa wa Mtwara  ambapo alichezea adi mwisho wa mashindano ,kufikia mwaka 1997 sheria ndani ya Tanesco zilipungua makali baada ya kutokea mabadiliko ya utawala hapo akarudishwa songea na akasajiliwa na Maji Maji suala ambalo lilimpa faraja kubwa sana ambapo alikitumikia kikosi hicho adi mwaka 2006.
Je?unafahamu baada ya mwaka 2006 alienda wapi?pia jumatano atasimulia jinsi alivyozuiwa kucheza Bandari mtwara na Tanesco.


Chapisha Maoni