Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





 
NGAO YA Jamii huko England ndio Mechi ya fungua dimba Msimu mpya na hushindaniwa kati ya Mabingwa Watetezi wa England na waliobeba FA CUP na safari hii Mabingwa Chelsea wataivaa Arsenal ambao walitwaa FA CUP Msimu uliopita.

 
Wakati Arsenal wakitinga kwenye mtanange huo wakiwa na matokeo mazuri kwenye Mechi zao za kabla ya Msimu za kugombea Barclays Asia Trophy huko Singapore na Emirates Cup Uwanjani kwao Emirates Jijini London na kubeba Makombe yote, Mabingwa Chelsea wao hawajashinda hata Mechi moja, ndani ya Dakika 90, katika Mechi zao za matayarisho.

 CHELSEA-PAREDI15
Katika Mechi hizo, Arsenal walipata ushindi mkubwa pale walipoichapa Lyon ya France 6-0 Uwanjani Emirates na pia kuitwanga Everton 3-1 huko Singapore.






Chapisha Maoni