Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Stivin Mapunda Garrincha wapili toka kushoto,mchezaji wa zamani wa simba,maji maji na Timu ya taifa stars.

Displaying mpira 2.jpg
  

“Sababu ya mimi kugombana na mwenyekiti wa Fat Mhidin Ndolanga chanzo ni kocha wa timu ya Taifa kipindi hicho, ambaye pia alikuwa kocha wa timu ya prisons ya mbeya Charles Boniface mkwasa kuwapanga wachezaji wa timu yake ya Prisons katika mechi ngumu nchini Rwanda kati yetu na Rwanga kwa kuwapa uzoefu wachezaji wake ili wafanye vizuri ligi kuu bara,na kuwaacha wachezaji muhimu nikiwemo mimi, ambao tulikuwa   wachezaji wazuri.


“Wakati mechi ikiendelea Ndolanga alimtuma mjumbe wake kuja kumuuliza kocha kwa nini mapunda hajaaza katika kikosi cha kwanza?,kocha alikaa kimya baadae akajibu ataingia,wakati huo hata wachezaji wezangu benjini walimwambia mapunda inatakiwa aingie akaokoe timu kwa kuwa tayari tulikuwa tumeshafungwa goli 1 hata hivyo kocha hakuchukua maamzi yoyote.
  
“Lakini zikiwa zimebaki dakika tano mpira kumalizika Mkwasa akaniita kwa Hasira nikapashe ili niingie nikaamua kukataa kwa kuwa muda ulikuwa umeisha hali hiyo ilimkasirisha  na akaamua kuandika ripoti ya jumla kuhusu mechi hile kuwa Mapunda alikataa kucheza tangu mwanzoni mwa mchezo, ali ambayo ilimfanya mwenyekiti wa Fat akasilike na kusema kuwa Sitacheza timu ya Taifa hadi hatakapo ng’atuka madarakani.

“Ugomvi wetu ulikuwa mkubwa hadi ukasababisha waziri Juma kapuya kumfungia Ndolanga kutokana na vurugu ambazo zilifanyika mara kwa mara kwa wadau na mashabiki wakishinikiza nicheze  mpira,lakini mara baada ya Ndolanga kurudi Madarakani na kukaa kiti kimoja kuzungumzia mgogoro wetu na yeye kujua Tatizo, mambo yote yakaisha na hadi hivi sasa mimi na Ndolanga ni  Marafiki wa kudumu.
Itaendelea…………..
 Endelea kufuatilia ambapo kesho tarehe 14 mwenzi 4 atasimulia kuhusu timu ya jeshi ya Botswana na simba itakuwaje? Uskose kusoma jelamba viwanjani.



Chapisha Maoni