Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


ENDELEA KUFUATILIA HISTORIA YA STIVIN MAPUNDA GARRINCHA AMBAPO JANA ALIISHIA KUSIMULIA, MGOGORO KATI YAKE NA MWENYEKITI WA FAT KIPINDI KILE SONGA NAE.

Displaying mpira 3.jpg

Garrincha wapili toka kushoto walioinama.

MECHI NINAYOIKUMBUKA

“Naikumbuka sana mechi ya Clab bingwa kati yetu Simba na Timu ya jeshi toka Botswana,mwaka2003 ili kuwa mechi muhimu kwetu na tulicheza katika kipindi kigumu ambapo wachezaji 5 muhimu wa simba walikuwa wamefungiwa na mimi nilipewa jukumu la ukepteni,mechi ambayo ilichezwa uwanja wa TaifA jijini Dar es salam,mechi  tulipata ushindi dakika ya 89 ya mchezo bao ambalo liliwekwa kimiani na mimi mwenyewe baada ya kubanwa sana na wapinzani wetu.

“Watu wengi wakizani kwamba mechi ya marudiano Tutatolewa kutokana na ushindi mwembamba ambao tuliupata nyumbani lakini mambo yakawa tofauti, tukiwa ugenini tulicheza kwa morali kubwa na tukafanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 3-0,na tukafanikiwa kusonga mbele amapo mechi iliyofuata tulipambana na Zamareck ya Misri mchezo ambao tulipata ushindi.

Mchezaji ninayempenda kwa sasa.

“Wachezaji wengi wanacheza vizuri lakini mtanzania anayekipiga Tp Mazembe nchini kongo Mbwana Samatta, nampenda sana ni mchezaji ambaye anatambua cha kufanya pindi awapo uwanjani.


Beki aliyekuwa anamsumbua

“kiukweli mabeki walikuwa wananiogopa,mara nyingi nilikuwa nakabwa na mabeki wane,watatu, kwa kuwa nilikuwa mtu hatari sana ,mabeki wote nilikuwa nawaweza.

Ushauri wake kwa Timu ya Maji Maji.

“Viongozi wazieshimu pesa za club,na waakikishe wanapigana hili kupata pesa za kuendeleza timu,kwa ajili ya maji maji.

“Hivi karibuni maji maji inatarajia kufanya uchaguzi wa viongozi wapya,ni wakati wa wanachama kuinusulu club ya Maji Mji kwa kuchagua viongozi wasio na uchu wa kutumia pesa za timu kinyume na Makubaliano.

Maisha Baada ya Soka

“Hivi sasa nimeoa na nina mke na watoto 3 na umri wangu ni miaka 36,namshukuru mwenyezi mungu kutonana na soka nafahamiana na watu wengi ambao wengi wao tunasaidiana katika maisha kiukweli mpira umenifungulia dira ya mafanikio yangu.


“Nina ofisi na najishugulisha na ukandarasi wa majengo pamoja na bara bara,lakini nafikiria kuwa na ofisi kubwa ili kuhakikisha najijenga vizuri zaidi kimaisha.


Zawadi kwa Watanzania.

“Nina mpango wa kujenga shule ya soka ‘sports academy centre’ambayo itafundisha mpira kuanzia ngazi ya chini ili kuwapata wachezaji wenye uwezo wa hali ya juu wa kucheza soka hapa nchini.

“Natarajia baada ya muda mfupi ujenzi utaanza kwa kuwa tayari taratibu za awali zimeshakamili na shule hiyo natarajia kujenga mkoani Ruvuma.alisema Garrincha.
Mwisho

Displaying mpira 1.jpg
Endelea kufuatilia mfurulizo wa makala za wachezaji AMBAPO WAMESTAAFU SOKA wa hapa Nchini waliowika nje na ndani ya TANZANIA.


Chapisha Maoni