Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Messi amefunga mabao 400


Mshambulizi wa Barcelona Lionel Messi amesema kuwa hakuwahi kufikiria kuwa atawahi kufunga mabao 400.
Mchezaji huyo aliyewahi kutwaa taji la mchezaji bora duniani mara nne aliwahi mabao mawili katika mechi yao dhidi ya Grenada vigogo hao wa ligi kuu ya Uhispania walipofunga mabao 6-0 .
Mshambulizi huyo wa Argentina alifunga mabao mawili ya 400- na 401.
Kocha wa Barcelona Luis Enrique alimsifu kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 akisema kuwa ilikuwa ni mafanikio makubwa.
Tangu atue Uhispania Messi ameifungia Barcelona mabao 359 akaifungia Argentina mabao 42 katika jumla ya mechi 506 alizoshiriki.
Kiungo huyo machachari ameisaidia sana Barcelona kutwaa mataji 21,yanayuojumuisha 6 ya ligi kuu ya Uhispania La Liga na 3 ya kombe la mabingwa barani Ulaya katika muongo mmoja uliopita.
Kibinafsi Messi alishinda mataji manne ya Ballon d'Ors,ambayo hutuzwa mchezaji bora duniani kuanzia mwaka wa 2009 hadi 2012.
"nitajitahidi zaidi kunogesha talanta yangu''


Chapisha Maoni