Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Alex Mapunda





Na Alex Mapunda,Iringa
SHIRIKISHO la soka hapa nchini TFF limesimamisha uchaguzi wa Lipuli ambao ulipangwa kufanyika Tarehe 28 Septemba[jana] baada ya kubaini kuwa katiba ya Lipuli ina mapungufu.
Akizungumza na JELAMBA VIWANJANI   mwenyekiti wa uchaguzi wa timu hiyo Jackson Ibrahim Chaula alisema taarifa ya kuhairishwa kwa uchaguzi waliipata masaa machache kabla ya uchaguzi huo ambapo kwa sasa wanaeshimu maamuzi ya TFF na wanasubiri marekesho  ya katiba hiyo.
“ni kweli kulikuwa na mapungufu ambayo yalikuwepo kwenye katiba ya timu ya Lipuli na marekebisho yalipelekwa Tff lakini Tff walichelewa kutupa  majibu,ambapo kwa sasa tulipanga kutumia katiba ya zamani suala ambalo Tff wamekataa.
Kwa upande wake kaimu mwenyekiti pia  mgombea wa nafsi ya mwenyekiti bwana Renatus Kalinga ilisema kuwa hizo ni nyama za watu wachache ambao wapo karibu na Tff wasioitakia mema timu ya Lipuli na wanatarajia kukaa kikao ili kujua hatima ya timu ya Lipuli kwa kipindi hiki ambacho inaitaji msaada mkubwa ikiwemo wao  kujiuzulu na kuwaachia wanachama wafanye maamuzi yao.

 Awali  uchaguzi huo ulitakiwa kufanyika  tarehe 28 mwenzi wa nane lakini wasimanizi waliamua kuahirisha kwa kuwa maandalizi hayakukamirika  lakini mwenzi huu imeshindikana tena suala ambalo linaweza likaigharimu timu hiyo kwa kuwa inaitaji usimamizi wa karibu sana, kuelekea kwenye kinyang’anyiro cha ligi daraja la kwanza mwenzi wa kumi.



Chapisha Maoni