Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




lipuli kicheko,kurugenzi kilio.
 
Na Alex Mapunda,Iringa
BAADA ya kufunya vibaya katika mechi zao za hawali timu ya Lipuli toka Iringa imezinduka usingizini na kuichakaza African Lyon kwa kichapo cha bao 1-0 katika mchezo wa ligi daraja la kwanza uliofanyika kwenye uwanja wa karume Jijini Dar es salam.
Katika mchezo huo ambao Lipuli walicheza kwa tahadhari kubwa kubwa ili kuepuka kufanya vibaya kwa mara nyingine bao pekee la Lipuli ambapo lilipeleka kilio kwa wapizani wao  lilifungwa na Abdala shauli na likadumu hadi dakika ya mwisho ya mchezo.
Hadi kufikia hivi sasa Lipuli imeshuka dimbani mara tatu ambapo mchezo wa kwanza walifungwa bao 2-1 dhidi ya Friends Rangers kabla ya kutoka sare na African Sports toka Tanga.
Kwa upande wa Kurugenzi wa mafinga wao wamejikuta wakikung’utwa bao 2-1 katika uwanja wao wa nyumbani dhidi ya wauza mitumba Ashanti United katika uwanja wao wa nyumbani na kuanza kupoteza matumaini ya kufanya vizuri kwa kuwa takwimu yao inaonyesha inashuka ambapo mchezo wa kwanza walishinda bao 2-0 dhidi ya Tessema Fc,mchezo wa pili wakatoka sare na mchezo wa mwisho wamechezea kichapo.
Kindumbwe ndumbwe cha ligi daraja la kwanza kimeanza kutimua vumbi mapema  mwenzi huu wa kumi ambapo safari hii kuna makundi mawili na Kundi A lina timu za African Lyon, African Sports, Ashanti United, Friends Rangers, Kimondo SC, Kurugenzi Mafinga, Lipuli, Majimaji, Mlale JKT, Polisi Dar es Salaam, Tessema FC na Villa Squad.

Wakati kundi B lina timu za Burkina Faso, Geita Veterans SC, Green Warriors, Kanembwa JKT, Mwadui SC, Oljoro JKT, Panone FC, Polisi Dodoma, Polisi Mara, Polisi Tabora, Rhino Rangers na Toto Africans. Ratiba ya Ligi hiyo itatolewa hivi


Chapisha Maoni