Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.






Na A lex Mapunda,Iringa

TIMU ya soka ya Lipuli imeamishia kambi yake Jijini Dar esalam ili kujianda vyema na michuano ya ligi Daraja la kwanza inayotarajiwa kutimua vumbi mapema mwenzi huu.
Akizungumza na JELAMBA VIWANJANI Katibu Msaidizi wa timu hiyo Ronjino Malambo alisema Timu ya Lipuli Ikiwa Dar es salam itacheza mechi za kirafiki ili kuimalisha zaidi kikosi cha timu hiyo ambapo wakati wa ligi Dar es salam watacheza mechi mbili na nyingine wataenda kucheza na African Sports mkoani Tanga kabla ya kurudi nyumbani Iringa ili kuendelea na michezo mingine.

“wadau tunawaomba sana wasitarajie miugiza  timu aiwezi kufanya vizuri bila wao kutoa michango ,sisi hatutaki pesa pekee hata mwenye mchele,ndizi,unga tunaomba atuletee ili timu iweze kufanya vizuri na kuutangaza vyema mkoa wa Iringa,kuhusu kambi ya jijini Dar kila kitu kimeenda vizuri hadi uwanja wa mazoezi tumepata”alisema malambo.

Kindumbwe ndumbwe cha ligi daraja la kwanza kinatarajia kutimua vumbi mapema  mwenzi huu wa kumi ambapo safari hii kutakuwepo na makundi mawili na Kundi A lina timu za African Lyon, African Sports, Ashanti United, Friends Rangers, Kimondo SC, Kurugenzi Mafinga, Lipuli, Majimaji, Mlale JKT, Polisi Dar es Salaam, Tessema FC na Villa Squad.

Wakati kundi B lina timu za Burkina Faso, Geita Veterans SC, Green Warriors, Kanembwa JKT, Mwadui SC, Oljoro JKT, Panone FC, Polisi Dodoma, Polisi Mara, Polisi Tabora, Rhino Rangers na Toto Africans. Ratiba ya Ligi hiyo itatolewa hivi punde.


Chapisha Maoni