Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




 MAHAKA ya hakimu mkazi kisutu jijini Dar es salam imeruhusu michuano ya miss Tanzania 2014 ambayo ilipangwa kufanyika kesho kutwa ifanyeke kama ambavyo ilipangwa.
 
Hakimu mkazi frank moshi ametoa maamzi hayo baada ya kusikiliza kwa makini ombi ambalo liliwasiliswa na mwazilishi wa mashindano hayo prashant patel,na kusema kuwa kusimamisha mashindano hayo kutawagharimu watu wasio na hatia wakiwemo wadhamini,hivyo hakuna umuhimu wa kusimamisha. 

MSHINDI wa shindano la Redd’s Miss Tanzania 2014 ataondoka na kitita cha sh. Mil.18 imefahamika.
Hayo yaMEsemwa leo na Meneja wa Kinywaji cha Redd’s Premium Cold  ambao ndiyo wadhamini wakuu wa shindano hilo Victoria Kimaro katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika  kwenye ukumbi wa JB Belmont Jijini Jijini  Dar es Salaam.
Kimaro alisema kwamba huu ni mwaka wao wa mwisho wa udhamini katika shindano hilo hivyo  wameamua kumpa mshindi fedha taslimu Mil.8 pia Mil. 10 ambayo ilikua anunuliwe gari nayo atapata fedha taslimu ili kama ataamua kununua gari ama kuweza kujilipia ada ya shule ama kufanya biashara hiyo itategea maamuzi ya mshindi huyo.
Kimaro anazitaja zawadi za warembo wengine kuwa ni atakayeibuka kuwa mshindi wa pili atapata kitita cha Mil.6, mshindi wa tatu atapata  Mil.4.2 mshindi wan ne atapata  Mil 3.2 wakati mshindi wa tano atapata Mil.2.2.
Warembo watakaoshika nafasi ya  6 hadi 15 wote kila mmoja taondoka na kitita cha Mil.1.2 huku wengine kuanzia wa 16 hadi 30 watapata kifuta jasho cha sh.700,000 kila mmoja alisema Kimaro.
Aidha aliongeza kwa kusema kuwa  katika shindano hili burudani kubwa itatolewa na msanii Omary  Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ na wapambe wake na mwanamuziki anayetamba hivi sasa Vanessa Mdee .
Kimaro amesema kwamba maandalizi ya shindano hilo yamekamilika huku ukumbi wa Mlimani City ukiwa katika hatua nzuri za maandalizi ikiwemo kutengeneza jukwaa la aina yake.
Aliongeza kwa kusema kuwa licha ya kuwa wao wanamaliza mkataba na Lino lakini mrembo atakayeshinda atapata stahili zote aikiwemo kupata posho za kazi mbalimbali za akijamii ambazo atakuwa akizifanya kabla ya kwenda kuiwakilisha nchi kwenye shindano la kumsaka mrembo wa dunia (Miss World).
Wakati huohuo Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International Agency  Limited ambao ndiyo waratibu wa shindano hilo Hashim Lundenga alisema kwamba tiketi zimeanza kuuzwa katika maduka ya vipodozi ya Shear Illusions, Mlimani City na Millenium Tower Makumbusho Jijini Dar es Salaam.
Jumla ya warembo 30 wanawania taji hilo ambalo linashikiliwa na Redd’s Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa.


Chapisha Maoni