Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




IRINGA

Na  Alex Mapunda,Iringa
Timu ya Lipuli toka mkoani Iringa imewadhiirishia wadau wa soka mkoa Iringa kuwa imepania kupanda ligi kuu baada ya kuwakung’uta watani wao wajadi Kurugenzi toka Mafinga bao 1-0 katika mtanange wa ligi daraja la kwanza uliofanyika kwenye uwanja wa Samora,juzi.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa mkali dakika zote 90,timu hizo zilianza kushambuliana zamu kwa zamu toka dakika ya kwanza lakini bahati ilikuwa kwa upande wa Lipuli  baada ya Jafari Hathumani Gonga kukwamisha mpira kimiani dakika ya 45 kwa ufundi mkubwa kwa faulo kufatia George mpole kumfanyia madhambi mchezaji wa Lipuli nje ya 18 ambaye alizawadiwa kadi nyekundu.
Kurungezi walikuja juu kwa kufanya mashambulizi langoni mwa Lipuli lakini walinzi wa Lipuli walikuwa Imara huku wakiakikisha  ngome yao haiteteleki ambapo hadi dakika 90 zilipokamirika Lipuli waliibuka kededea kwa ushindi wa bao 1-0.
Kivutio kikubwa katika mchezo huo walikuwa ni mashabiki wa timu ya Lipuli wakiongozwa na Salum Kisako ambao wanauchu wa kuona timu yao ikipanda ligi kuu ambapo walishangilia kwa muda wote huku wakisema hawawezi kufungwa na wakata magogo toka Mafinga.
Baada ya kumalizika mchezo huo Kaimu mwenyekiti wa Lipuli Renatus Karinga  alitoa maneno makali ya kisoka kuwa Lipuli ikifungwa na Kurugenzi ataachana na masuala yanayohusu kandanda,huku akiwa amejawa na furaha kubwa ya ushindi.
Lipuli sasa imefikisha pointi 20 ponti 1,nyuma ya Friend Rengers ambao nao wamemaliza mechi zao za mzunguko wa kwanza.


Chapisha Maoni