Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


 


Real Madrid wamefuzu hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya lakini "kimkanda mkanda" baada ya kuchapwa mabao 4-3 na wageni wake Schalke 04.



Madrid imefungwa nyumbani baada ya ushindi wa mabao 2-0 ugenini nchini Ujerumani hivyo kufanya ifuzu kwa jumla ya mabao 5-4.

Mashabiki wake, waliwazomea wachezaji hao wakati wakiboronga na kufungwa na Madrid walifanikiwa kusawazisha mara tatu, lakini wakashindwa kufanya hivyo mara ya nne.

Mshambuliaji wake, Cristiano Ronaldo alifanikiwa kufunga mabao mawili, lakini akashindwa kuonyesha cheche kabisa.

Mashabiki walionyesha kutofurahia uchezaji wa timu hiyo ambao ndiyo mabingwa watetezi kufuzu kwa hofu.





Chapisha Maoni