Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Jumanne Usiku Robo Fainali za UEFA CHAMPIONZ LIGI zitaanza kwa Mechi mbili na moja ikiwa huko Jiji la Madrid, Spain ndani ya Estadio Vicente Calderon wakati Atletico Madrid watakapokuwa Wenyeji wa Mahasimu wao Real Madrid.
Mechi hii, Dabi ya Madrid, maarufu kama El Derbi Madrileño, ni Marudio ya Fainali ya Msimu uliopita ya UEFA CHAMPIONZ LIGI ambayo Real Madrid waliinyuka Atletico Madrid Bao 4-1 na kutwaa Ubingwa wa Ulaya kwa mara ya 10.
Mechi nyingine ya Jumanne Usiku itachezwa huko Jiji la Turin Nchini Italy wakati Wenyeji Juventus watakapoivaa AS Monaco ya France.
TATHMINI
Kila Timu itaingia kwenye Mechi hii ikidhamiria kisasi.
Kwa Atletico, kisasi chao ni kile cha kufungwa na Real kwenye Fainali ya Mashindano haya huko Lisbon Msimu uliopita na kwa Real ni kubondwa mara 4 na Sare 2 na Atletico tangu Fainali hiyo.
Vipigo kwa Real ni pamoja na kutupwa nje ya Spain Supercup na Copa del Rey.
Katika pambano lao la mwisho Mwezi Februari, kwenye Mechi ya La Liga, Atletico iliitwanga Real 4-0 ikiwa ndio ushindi wao mkubwa dhidi ya Wapinzani wao wakubwa katika Miaka 28.
Hilo limemfanya Kocha wa Real, Carlo Ancelotti, aseme: "Matokeo ya mwisho na Atletico ndio yanatupa motisha sisi!" 
Lakini, tofauti na Mechi zilizopita Msimu huu, safari hii Real watatinga kwa maadui zao Vicente Calderon wakiwa na Kikosi kamili kwa mara ya kwanza katika Miezi Mitano.
James Rodriguez na Toni Kroos,  ambao waliikosa Mechi ya La Liga ya Jumamosi walipoifunga Eibar 3-0 baada ya kuwa Kifungoni, wanarejea dimbani.
Nao Atletico wana habari njema ya kurejea dimbani baada ya kuzikosa Mechi mbili akijiuguza Enka kwa Straika wao Mario Mandzukic ambae tangu ahamie Atletico akitoka  Bayern Munich mwanzoni mwa Msimu amepachika Bao 20 zikiwemo Bao 2 katika Gemu mbili dhidi ya Real Uwanjani Vicente Calderon. 
Jumatano pia zipo mechi mbili nyingine za Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI kati ya PSG na Barcelona huko Mjini Paris na nyingine itachezwa huko Ureno kati ya FC Porto na Bayern Munich.
VIKOSI VINATARAJIWA:
Atletico Madrid: Oblak; Juanfran, Miranda, Godín, Gámez; Arda Turan, Tiago, Suárez, Koke; Griezmann, Mandžukić.
Real Madrid: Casillas; Carvajal, Pepe, Ramos, Marcelo; Kroos, Modrić, James; Bale, Benzema, Ronaldo.
REFA: Milorad Mažić (Serbia) 
UEFA CHAMPIONZ LIGI
Robo Fainali-Mechi za Kwanza
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku, Saa za Bongo
Jumanne Aprili 14
Atlético Madrid v Real Madrid
Refa: Milorad Mažić (Serbia) – Uwanja: Estadio Vicente Calderón, Madrid, Spain
Juventus v AS Monaco
Refa: Pavel Královec (Czech Republic) – Uwanja: Juventus Stadium, Turin, Italy
Jumatano Aprili 15
Paris Saint-Germain v Barcelona
Refa: Bado kujulishwa– Uwanja: Parc des Princes, Paris, France
FC Porto v Bayern Munich 
Refa: Bado kujulishwa – Uwanja: Estádio do Dragão, Porto, Portugal
UEFA CHAMPIONZ LIGI
Robo Fainali-Mechi za Marudiano
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku, Saa za Bongo
Jumanne Aprili 21
Bayern Munich v FC Porto [Allianz Arena, Munich, Germany]
Barcelona v Paris Saint-Germain [Nou Camp, Barcelona, Spain]
Jumatano Aprili 22
Real Madrid v Atletico Madrid [Santiago Bernabeu, Madrid, Spain]
AS Monaco v Juventus [Stade Louis II, Monaco, France]


Chapisha Maoni