Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





 Na Ally Ruambo.
TIMU ya Vijana   chini ya miaka  12 kutoka wilayani kilwa  wanatarajiwa kuondoka nchini kuelekea nchini Finland  kushiriki katika mashindano ya mpira wa miguu(min football) yanayojumuisha vijana chini ya miaka kumi na mbili. 

Mashindano hayo  ambayo hufanyika nchini finland kila mwaka ambapo wilaya moja nchini Tanzania huchaguliwa kuunda timu ambayo inaenda kuiwakilkisha nchi katika mashindano hayo  nchini finland.

Wachezaji hao kumi na mbili wanaounda timu hiyo wamepatikana katika mchujo ambao ulikutanisha wanafunzi mbali mbali toka shule tofauti za msingi kutoka wilayani hapo chini ya mpango unaojulikana kwa jina la ELIMU NA MICHEZO ambapo FC VITO kutoka nchini finland kwa kushirikiana na wizara ya elimu Tanzania wanaratibu mpango huo. 

 Timu hiyo inaenda kushindana katika mchezo ambao unajulikana kama min football ambao unakua tofauti kidogo na mpira wa miguu amabao tumeuzoea ambapo idadi ya wachezaji wa ndani wanakua pungufu, wanakua 7 pia vipimo vya uwanja vinapungua ukilinganisha na mpira wa miguu wa kawiada.
 
Timu ya vijana chini ya miaka kumi na mbili kutoka wilaya ya kilwa katika picha ya         pamoja na viongozi mbalimbali mara baada ya kukabidhiwa bendera ya nchi.
Akizungumza na mwandishi wetu afisa michezo wilaya ya kilwa ndugu Mtule amesema timu iko katika hali mzuri imefanya maandalizi ya kutosha na vijana wana morali ya mashindano na anaamini watafanya vizuri. 

 “Vijana walikua  wengi  ambao wana viwango vizuri lakini tumewaacha kwa kigezo cha umri kwa sababu wana  umri ambao umezidi miaka kumi na mbili kitu ambacho ni kinyume na kanuni za mashindano ambapo wachezaji wanaotakiwa ni chini ya umri wa miaka kumi na mbili pia walikua wengi lakini waliokua wanahitajika ni kumi na mbili tu.” Alisema Mtule.

Pia ameongeza kua wamekumbana na changamoto nyingi lakini changamoto kubwa ni  baadhi ya wazazi wachache hawakua tayari kuwapa ruksa watoto wao kwa safari ya kuelekea finland mara baada ya kuchaguliwa   kwahiyo wakaamua kuwaacha na kuwachagua wengine ambao wana uwezo na wako tayari kwa  safari.
Kwa upande wa wachezaji wamesema wako vizuri kwani wamefanya mazoezi ya kutosha kwahiyo wanakwenda nchini finland kushindana na kuhakikisha wanarudi na ushindi kwa taifa letu.

Mapema jana vijana hao walikabidhiwa bendera ya nchi na mkuu wa wilaya ,wilaya ya kilwa Mh. ABDALLAH ULEGA Katika hafla fupi ya kuiaga timu hiyo  iliofanyika katika viunga  vya majengo ya halmashauri ya wilaya ya kilwa  ambapo viongozi kutoka idara mbali mbali,viongozi wa dini, kamati ya ulinzi na usalama ,wanafunzi pamoja na ndugu na jamaa wa wachezaji hao wali udhuria katika hafla hiyo.

Msafara wa  timu hiyo  pamoja na afisa michezo  wa wilaya  umeanza  safari leo alfajiri kutoka kilwa  kuelekea jijini dare s salaam ambapo mara baada ya kufika dar es salaam watatembelea   ubalozi wa finland nchini tanzania  kabla ya kuanza safari kuelekea nchini finland mapema wiki hii ambako mashindano yanatarajia kufanyika.

Mdau mkubwa wa michezo wilayani kilwa Hamisi Kassinge kataka picha ya pamoja na baadhi ya wachezaji.







Chapisha Maoni