Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



BARCABINGWA2015LEO Shirikisho la Soka huko Spain, RFEF, wametoa Ratiba ya Msimu mpya wa 2015/26 ambao utaanza Agosti 22.
Ile Mechi, Bigi Mechi huko Spain iliyobatizwa El Clasico, kati ya Mahasimu Barcelona na Real Madrid, itapigwa Novemba na Marudiano ni Aprili.
El Clasico ya kwanza itakuwa Santiago Bernabeu hapo Novemba 8 na Marudiano ni Aprili 3 huko Nou Camp.
Dabi ya Jiji la Madrid, iliyobatizwa El Derbi Madrileno, kati ya Real na Atletico Madrid itachezwa huko Vicente Calderon Nyumbani kwa Atletico hapo Oktoba 4 na Marudiano ni Santiago Bernabeu Februari 28.
Agosti 22, Siku ya Ufunguzi ya Mechi za La Liga, Real, wakiwa chini ya Meneja mpya Rafa Benitez, wataanza Msimu wao Ugenini kwa kucheza na Timu iliyopanda Daraja Sporting Gijon huko El Molinon Stadium huku 
Mabingwa Barcelona wakianza Ugenini na Athletic Bilbao lakini hiyo itakuwa mara ya 3 kwa Timu hizo kukutana kwani wao ndi watafungua dimba Msimu huko Spain kwa kugombea Super Cup hapo Agosti 14 na kkurudiana Agosti 17.
MECHI ZA SIKU YA UFUNGUZI:
Athletic Club vs. Barcelona
Malaga vs. Sevilla
Levante vs. Celta Vigo
Sporting Gijon vs. Real Madrid
Rayo Vallecano vs. Valencia
Espanyol vs. Getafe
Deportivo vs. Real Sociedad 
Granada vs. Eibar
Real Betis vs. Villarreal
Atletico Madrid vs. Las Palmas  


Chapisha Maoni