Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Athletic Bilbao 4-0 Barcelona: Lionel Messi and co shocked by half-way line stunner before




Siku chache baada ya kutwaa ubingwa wa Uefa Super Cup, Barcelona wamekiona cha moto baada ya kukutana na kipigo cha mabao 4-0 kutoka kwa Athletic Bilbao.

Licha ya kuwemo kwa nyota Lionel Messi, Bilbao wametoa adhabu hiyo kwa Barcelona katika mechi ya Super Cup ya Hispania.

Hadi mapumziko, Bilbao walikuwa wanaongoza kwa bao 1-0 lililofungwa na Mikel San Jose aliyefunga katika dakika ya 13.

Huku ikionekana Barcelona ingerejea na kujirekebisha katika kipindi cha pili kama ilivyofanya kwenye mechi ya Uefa Super Cup dhidi ya Sevilla baada ya kutangulia kufungwa na kusawazisha, haikuwa hivyo.

Kwani Bilbao ndiyo walizidi kupaa na kufunga mabao ya harakaharaka baada ya Artiz Aduriz kufanya mabao mawili ya fasta katika dakika ya 53 na baadaye 63.

Kitendo cha Bilbao kufikisha mabao matatu kilionekana kuwachanganya Barcelona, wakaendelea kushambulia mfululizo na kujisahau kufanya ulinzi mzuri.

Hali hiyo ilisababisha Bilbao kupata bao la nne kupitia Aduriz aliyekuwa anafunga lake la tatu au hat trick.

MATCH FACTS 

Athletic Bilbao: Iraizoz, Laporte, San Jose, Balenziaga, Etzeita, Benat, Susaeta (Boveda 85 mins), Eraso (Gurpegi 77), De Marcos, Sabin (Lekue 66), Aduriz 
Subs not used: Iago, Elustondo, Aketxe, Kike 
Booked: Etxeita, San Jose, Benat, Eraso, Susaeta, Gurpegi 
Goals: San Jose 13, Aduriz 53, 62, 68 
Barcelona: Ter Stegen, Alves, Vermaelen, Bartra, Adriano, Mascherano, Rafinha (Iniesta 52), Sergi Roberto (Rakitic 60), Messi, Suarez, Pedro (Sandro 71)
Subs not used: Bravo, Pique, Busquets, Munir 
Booked: Alves, Mascherano, Pedro, Iniesta 




















Chapisha Maoni