Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Van-der-Sar
Kwa sasa hawapo tena kwenye tasnia hii ya soka, lakini mchango wao utabaki katika vitabu vya historia. Walijitahidi kadri walivyoweza kuhakikisha timu zao zinafurahia mafaniko iwe kwenye ligi za ndani ama michuano ya Ulaya. Kutokana na utangulizi huo, hawa ndio wachezaji watano bora ambao wamewahi kucheza michezo ya UEFA wakiwa na umri mkubwa.
 
5. Edwin van der Sar–miaka 40 na siku 212
FC Barcelona v Manchester United FC, 28/05/2011
“Mara nyingi unakuwa na ndoto za kucheza katika timu yako ya taifa lakini vile vile kunyakua ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya,” alisema.
 
4. David Weir–Miaka 40  na siku 212 
Bursaspor v Rangers FC, 07/12/2010
“Sifikirii kuhusu hilo; nadhani hilo ndio jibu fupi kiukweli,” aliiambia UEFA.com.
“Najifikiria mwenyewe kama moja ya wachezaji. Sivutiwi na umri wangu lakini nimekuwa nikijibu kuhusu hilo kwa kipindi kirefu sasa na kuona kwamba suala hili kamwe halitabadilika.”
 
3. Alessandro Costacurta-miaka 40 na siku 213 
AEK Athens FC v AC Milan 21/11/2006
 
Alishinda mataji 23 katika maisha yake ya soka, huku mataji mengi akivuna pindi akiwa na klabu ya Ac Milan. alicheza michezo 458 akiwa Ressoneri, akishika nafasi ya tatu miongoni mwa wachezaji waliocheza michezo mingi zaidi klabuni hapo. Alistaafu akiwa amecheza michezo 660 kunako ligi ya Serie.
2. Mark Schwarzer- miaka 41 na siku 198
Club Atlético de Madrid v Chelsea FC, 22/04/2014
Mchezaji huyu wa zamani wa timu ya taifa ya Australia alikuwa mchezaji wa kwanza mwenye umri mkubwa kucheza kwa mara ya kwanza kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati Chelsea ilipoinyuka timu ya Steaua BucureÅŸti bao 1-0. 
“Ulikuwa ni mchezo mkubwa sana kwangu na nimefurahi sana kwa kitendo cha kocha kuniamini na kunipa nafasi ya kutimiza ndoto za maisha yangu za kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya,” Schwarzer aliiambia UEFA.com.
1. Marco Ballotta- 43 years and 253 days
Real Madrid CF v SS Lazio, 11/12/2007
“Wakati nikiwa kijana mdogo niliambiwa kufanya juhudi ili nikuze kiwango; na sasa nina umri mkubwa, naambiwa kuongeza juhudi kutokana na umri wangu kuwa mkubwa,”
“Hakuna siri juu ya hili. Unatkiwa kupewa motisha, lakini jambo kubwa zaidi ni kuwa na furaha wakati wote, iwe mazoezini au kwenye mechi. Kutokuwa na majeraha ya mara kwa mara, nadhani utapata jibu juu ya hilo.” alisema Marco. Alistaafu rasmi mwaka 2008.


Chapisha Maoni