Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





Na Alex mapunda
25-03-2014

Maji maji FC.
 Miongoni mwa Timu ambazo zilitokea kuwa tishio hapa nchini miaka ya 1980 hadi 2000 ukiziweka kando  Simba na Yanga utakubariana na mimi kuwa Maji Maji ya Songea Maarufu kwa Jina la Wanalizombe ilikuwa tishio hapa nchini.

Maji Maji ambayo Ilizaliwa rasmi mwaka 1977 kwa muunganiko wa timu mbali mbali mjini Songea chini ya Mwasisi wa timu hiyo Dk Roulence Gama ilianza kupata umaarufu mkubwa mwaka 1980 mwaka ambao timu hiyo ilipata nafasi ya kushiriki kwa mara ya kwanza ligi Daraja la kwanza hapa nchini.
Licha ya kuwa na uwezo mzuri uwanjani na kusajii wachezaji wazuri Maji Maji haikubaki nyuma kwa kuamini Imani za kishirikina,imani ambazo zimetayala soka la Tanzania tangia miaka ya nyuma,Jelamba Viwanjani baada ya kufanya utafiti wa kina imefanikiwa kunasa baadhi ya matukio ya kishirikina ambayo yametokea katika klabu hiyo kupitia kwa wachezaji na viongozi ambao wamewai kutumikia timu hiyo katika nyakati tofauti,  kama wanavyofafanua ;-

ALLY MCHUMILA


Displaying aliy mchumila.jpg




     Wakati natumikia Maji Maji kama Meneja mchezaji  nakumbuka Tulimsajili Mzee wa kamati ya ufundi  nje ya uwanja toka Afrikan Sports Mzee ambaye alikuwa na uwezo wakusimulia matukio yote ya uwanjani wiki moja kabla ya mchezo na wao aliwapa ubingwa,ambapo baada ya kumsajili  tulienda kucheza na Yanga Jijini Dar es salam mchezo ambao ilikuwa mgumu sana kwetu  lakini Yule mzee wiki moja kabla alituambia  kuwa  Yanga Tutawafunga Bao 1-0,bao ambalo litafungwa na beki sio mshambuliaji.

    Kweli mchezo ulikuwa mgumu sana kwa pande zote lakini mimi na viongozi wenzangu tulijiamimi sana kwa kuwa mtaalaum Alisha tuambia matokeo ya mchezo, ambapo kama alivyosema Yule Mzee beki wa Maji Maji Piter Mhina aliwafunga midomo mashabiki  wa yanga kwa kufunga bao safi ambalo lilidumu hadi dakika  90 za mchezo zipomalizika.

 SHAIBU KAMBANGA

 

Displaying shaibu kambanga.jpg










''Mwaka 1996 mzee wa timu ya Maji Maji sitamtaja jina kwa kuwa namweshimu sana alituita chumbani na kutufunika shuka nyeupe akaanza kupiga Manyanga mimi nilikuwa nimekaa na marehemu Kisochi lemba mzee alikuwa anaongea lugha ambayo hakuna aliyekuwa anaielewa lakini ilikuwa kila akipita nilipo mimi nilisika neno la mwisho akisema Maji Maji tufungwe tatu na Simba nilijaribu kumweleza mwezamu yeye akasema sio kweli ila mzee kasema Maji Maji tushinde tatu,niliendelea kumsikiliza yule mzee kwa makini sana na baada ya tukio lile nilijalimu kuwaeleza wenzangu wote walishangaa.

 ''Tukaja kwenye mechi mchezo ulikuwa mgumu sana upande wetu na kama yule mzee nilivyomsikia mimi Simba walitubugiza bao 3-0

KENNETH WANE







Displaying kennethwanne.jpg


“Tukio hili hadi naingia kaburini siwezi kusahau,nakumbuka mwaka 1995 tulienda mwanza kucheza na Pamba ya mwanza viongozi wa Maji Maji wakatupeleka kwa mganga wa  Toto Afrika ili kutufanyia dawa kwa kuwa toto na pamba walikuwa wapinzani wakubwa.

“Siku hiyo tulichanjiwa dawa na kila mmoja aliogeswa dawa Ndoo mbili na tulipelekwa wachezaji 7,lakini mimi sikufurahishwa na kitendo cha kuchanjwa dawa nikamua kumdanganya mganga ili asinichanje nilichokifanya nikamwita pembeni na kumwambia kuwa wakati nipo mdogo nilipatwa na ugonjwa wa ajabu na wazazi wangu wakanipeleka nchini msumbiji ili kunifanyia dawa ambapo mganga wa msumbiji alinichanjia dawa na akaniambia mtu yeyote arusiwi kunichanjia dawa hadi kitoke kibari toka kwake  baada ya kumweleza hayo mganga akaduwaa!

“ baadae akanipa ilizi ambayo niliiweka kwenye ugoko ,pia baada ya kuoga dawa mganga alituagiza tukatafute kuku na kumchinja saa saba usiku na damu yake kuchanganywa na maji pia kuoga kitu ambacho tulikitekeleza,lakini baada ya Dakika 90 za mwamuzi kukamirika pamba 5-1,ali ambayo ilitufanya tutoke uwanjani vichwa chini.

 ISIHAKA MAJALIWA

Mwaka 1983 kulikuwepo na mechi kali sana kati yetu na Simba toka jijini Dar es salam mechi hile ilichezwa wakati kamati ya ufundi ya Simba ilikuwa inaongozwa na kikosi ambacho kilikuwa imesheni vichwa toka Brazil na wakati tunakutana nao Simba ilikuwa imezindua mfumo mpya wa kibrazili maarufu Kama ‘Kanivo Samba’ hakika simba ile ilikuwa inatisha.

“Nikiwa kipa namba 1 wa timu  yetu Viongozi wakanichukua na kunipeleka kwa  Mganga wa jadi ambaye sasa ni Marehemu ili kuchukua mbinu za kuidhibiti Simba.

“Wakati wa asubuhi  nakumbuka mganga aliniambia kuwa, mechi itakuwa ngumu sana kutokana na uimala wa wapizani wetu,usiku wa leo nimejitaidi kuokoa magoli mengi sana kadili ya uwezo wangu lakini hata hivyo yamebakia magoli mawili ambayo nitayamalizia uwanjani wakati mechi ikiendelea.

“Wakati wa mchezo ulipowadia timu zote zikaingia uwanjani na mechi ikaanza,mechi ilikuwa ngumu sana na Simba walipata bao 2 za wazi lakini waamzi wa mchezo ule akayakataa na kusema wafungaji waliotea[off side] na hadi mwisho wa mchezo  tukatoshana nguvu ya bila kufungana,hapo ndipo nikakumbuka maneno ya mganga na kuamini uwezo wake.

 JOHN KABISAMA

“Mwaka 1985 kulikuwa na pambano kali kati ya maji maji na Pan Afrika pambano ambalo ilitakiwa lichezwe siku ya Jumamosi lakini pan walichelewa kufika uwanjani kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi na pambano likahailishwa adi siku ya Jumatatu.

“Kipindi hicho Maji Maji alikuwa imemuleta mzee wa kamati ya ufundi Toka Kigoma ambaye alikuwa anahakikisha kamati ya ufundi nje ya uwanja inakwenda sawa.

“Yule Mzee tulimpa jina la Mzee Mziba jina la mchezaji maarufu kutokea kigoma,kwa kweli mimi nilikuwa siamini imani hizo lakini yule mzee nilimweshimu sana,nakumbuka alituambia kuwa  mechi yetu na Pan itachezwa siku ya Jumatatu tutashinda bao 3-0,na hata kama tukipata nafasi nyingine ya kufunga bao haitawezekana.


 “kwa kipindi kile Pan Afrika likikuwa Tishio Mimi sikuafiki kama tungeweza kupata ushindi mkubwa kiasi kile lakini sisi tulikuja kuamini mara baada ya kumalizika ule mpambano ambapo tulishinda bao 3-0 kama alivyotuambia yule mzee,hali ambayo ilinishanganza sana.
 Pia yule mzee mwaka 1985 alitabili mchezo wetu dhidi ya simba kuwa tungeshinda bao 2-1 kitu ambacho kweli kilitokea ambapo yule mzee alituwezesha maji maji kuchukuanubingwa mwaka 1985 kutokana na ubora wa dawa zake.

GOD MVULA.






Displaying god mvula.jpg



 “Baba yangu alikuwa mkurugezi wa Matimila Bendi pia ilikuwa karibu sana na Mzee gama  kipindi hicho nipo shule ya msingi  kulikuwa na wimbo ambao ilitungwa na Amza Clara chini ya bendi yake,wimbo ambao ulifahamika kwa jina la mchaka Mchaka.
  
“Wimbo wa mchaka mchaka uliusishwa na imani za kishirikina ulikuwa ukipigwa lazima lazima Maji Maji Ipate ushindi pia ilichochea Morali kubwa kwa timu ya Maji Maji na ikapelekea kupata umaarufu mkubwa.



Displaying MAJI MAJI SC 1998.jpg









 Kwa matukio hayo machache licha ya Maji maji ya hivi sasa kukumbwa na tatizo la uchumi tatizo ambalo linaelezwa ni chanzo kikuu cha timu hiyo kufanya vibaya kuazia mwaka 2000 hadi hii leo pia unaweza kukubariana na mimi kuwa kamati ya ufundi ya kuimalisha timu hiyo imekosa wataalam kama akina mzee mziba ambao waliifanya kazi hiyo kwa kiwango cha hali ya juu sana.
 Ujenzi wa Maji maji mpya.
Pia maji maji ya sasa ili iweze kurudisha makali yake ya zamani lazima wanaruvuma wote waweke shida zao chini na kurusha mikono juu, huku wakisahau tofauti zao pasipo kujali itikadi,dini,ukabira,siasa na hata jinsia kinyume na hapa maji maji itaendelea kubaki kichwa cha mwenda wazimu,huku wakimsaka mchawi wa timu hiyo wakati wachawi ni wenyewe.



Displaying b.jpg


















Chapisha Maoni