Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




 ALI YUSUPH SULEMAN TIGANA ALIKUWA MCHEZAJI NYOTA HAPA NCHINI

ILIPOISHIA JANA…….:-

“hiyo ni 9 kakini 10 wakati tuliposhuka uwanja wa ndege jiji Dar es lalam hapo tulinyong’onyea kabisa kwa kuwa tulipokea Taarifa ya kwamba mchezaji wa Mahili wa Soka Ramadhani Lemi alikuwa amefariki dunia’anavuta pumzi na machozi yakamtoka kutokana na kukumbuka jinsi ilivyokuwa’kisha anaendelea kusimulia; kiukweli majonzi ambayo tulikuwa nayo ni makubwa sana basi moja kwa moja tukaenda kwenye mazishi ya mchezaji mwenzetu,mungu awaweke mahali pema peponi wale wote ambao walipoteza maisha siku ile.


 SONGA NAYO..........................


Nilikimbia na laki moja ya Dewji.


“wakati nipo Pan Afrika kuna kipindi tulicheza mechi ya kirafiki na wekundu wa msimbazi Simba,mchezo ambao nilicheza kwa kiwango cha hali ya juu sana hali ambayo ilipelekea viongozi wengi wa simba kunimezea mate ambapo baada ya mchezo ule, aliekuwa mdhanini wa simba Azim Dewji aliwatuma watu wake kunitafuta ambapo walikuja hadi nyumbani na wakanichukua na kunipeka ofisini kwake.



“siku ya kwanza kuingia ofisini kwa Dewji niliogopa sana kwa kuwa sikuwai fikilia kama kuna siku nitafanikiwa kuingia ofisini kwake kwa kuwa Dewji alikuwa Tajiri mkubwa,baada ya kuingia ofisini kwake alinipokea vizuri na akaniambia kuwa ameridhika na uwezo wangu wa uwanjani na alinitaka kusaini Simba,nilijifikiria sana kabla ya kumjibu kwa kuwa Pan Afrika walikuwa wamenifadhili mambo mengi sana hivyo nilifikiria juu ya kusaini simba bila kuwalipa fadhira zao,kwa woga nilimkubalia dili la kusaini Simba.





“basi Dewji akanipa kitita cha shiringi laki moja pia akiniambia kuwa anasafari ya kwenda uingereza  hivyo akirudi tutakamilisha kila kitu,kiukweli moyoni nilikuwa njia panda na uamzi ambao nilipanga kuuchukua baada ya kufikiria kwa kina ni kuchezea Pan Africa kwa kuwa tayari nilikuwa na mkataba nao.



“Dewji baada ya kutoka Uingereza alinitafuta sana ili kusaini mkataba Simba kwa kipindi hicho aliwatuma watu wake lakini nilikuwa nikiwapiga chenga kwa kuwa kipindi kile mawasiliano yalikuwa magumu nilifanikiwa kuwatoroka adi msimu uliponza nikavaa uzi wa Pan Afrika.


 Itaendelea kesho tarehe 24-04-2014 atasimulia kuhusu imani za kishirikina uwanjani na zaidi kuhusu tukio la kulewa pombe nchini Zimbabwe.



Itaendelea……………..


Chapisha Maoni