Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


TAREHE 3-4-20104

Displaying IMG_0290.jpg

 JUMATATU ALIISHIA AKIWA NA MAJI MAJI MWAKA2006 SONGA NAYO ILI KUFAHAMU MENGI

Mwaka  2007 alipata uhamisho kikazi kwenda mbinga  hapo ndipo ukawa mwisho wa kuitumika maji maji lakini alijiunga na Mbinga United  timu ambayo ameichezea hadi mwaka jana 2012 ambapo kwa sasa amestaafu kucheza soka la ushindani,na anachezea timu za veteran,anasimulia Hamis Mtepa Kisha anaendelea;-

Nilizuiwa kuvaa jezi ya Bandari Mtwara.

“wakati Tanesco waliponiamishia Mtwara kikazi timu ya baadari walilidhika  na uwezo wangu na walitoa donge nono kunisajili lakini Tanesco walinizuia na kauli ilikuwa ni ile ile kwamba asietaka kufanya kazi Tanesco akacheze mpira, sikuwa na  jinsi niliishia kufanya nao mazoezi pekee ingawa kwa kipindi kile ilikuwa bahati kubwa sana kuchezea timu ambayo ilikuwa na jina kubwa kama Bandari ya Mtwara,na atimayenikaishia kuchezea timu za mtaani.

Mechi Kali.

“siwezi kusahau mechi  kati ya Tanesco dhidi ya Yanga uwanja wa Maji Maji  mjini Songea ,kwangu mimi ulikuwa ni mchezo wa kwanza kusimama langoni dhini ya Timu kubwa na ukizangatia kwa upande wa Yanga ilikuwa mechi yao ya kwanza mara baada ya kuchukua ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati nchini Uganda mchezo ulikuwa mgumu  sana kwa kuwa tulikutana na wachezaji wenye  majina makubwa kiasi kwamba tulikuwa tukiyasikia Radioni pekee.

“tulijitaidi sana kipindi cha kwanza tuliwashindilia yanga bao moja kwa nunge lakini kipingi cha pili mambo yakabagilika kama waswahili wasemavyo mtoto mdogo  alali na pesa Yanga walitukimbiza sana ambapo walifanikiwa kupata mabao mbili yaliyowekwa kimiani na Mahamed Husein Maarufu kama mmachinga hadi mwisho wa mchezo yanga waliibuka na ushindi wa bao 2-0.

Ushirikina
“Mambo hayo kwenye mpira yapo  lakini kwa kiasi kikubwa uchangia kushuka kwa ufanisi katika timu kwa kuwa viongozi wa timu badala ya kuwalipa wachezaji vinzuri  wanajiziuka na imani za kishirikina,kuna kipindi Maji Maji walimsajili mchezaji Idifonzi Hamlima  toka Mtwara mchezaji ambaye alikuwa tishio kwa soka la hapa mchini baada ya kutua Maji Maji akacheza chini ya kiwango kwa makusidi na akasema awezi kutumia nguvu nyingi wakati ujira mdogo.

SIKU 100 za Malinzi amesahau kusini.
“Moja ya maeneo ambayo yana vipaji halisi vya mpira uwezi kusahau mkoa wa Ruvuma na nyanda za juu kwa ujumla, lakini katika siku Mia za utawala wa Rais mpya wa Shirikisho la Soka hapa nchini ajakakanyaga Ruvuma hii inaashiria kuwa mchango wa mkoa wa Ruvuma wa kutoa wachezaji wenye vipaji vya soka hapa nchini kwa sasa hautambuliki ndio maana mtu wa mwisho kuchezea taifa Stars kwa Mafanikio Toka Ruvuma ni Stivin Mapunda Garincha,

“Lakini ndani ya siku hizo 100 tayari malizi ameshaenda mikoa ya kasikazini hivyo namshauri Rais wa wa soka ili kuendeleza soka la hapa nchini kwa vitendo lazima afanye ziara kanda zote na kuchukua maoni ya wadau wa soka na kufanyia kazi.

Nilipenda kuchezea Simba sikupata nafsi.

“mimi naipenda Simba toka nikiwa mdogo kiasi kwamba  nilijitaidi kucheza kwa bidii ili samba wanichukue lakini mambo yakawa kinyumbe kabisa sikupata ofa yeyote ya kusajiliwa na samba,hata kuwasikia watu mtahani nataka kusajiliwa na samba sikusikia kabisa,lakini adi leo mimi ni Simba damu.

Soka la zamani na sasa.

“zamani tulikuwa tukicheza kwa moyo wote,ilikuwa faraja sana kwa mchezaji kuingia uwanjani ukiwa umevaa jenzi huku ukitumia timu yako kwa dhati bila kujali malipo,lakini wachezaji wa siku hizi ingawa awafanani na pesa wanayochukua ni wavivu sana tukilinganisha na zamani.

Nilitema mpira nikafungwa.
“kila nikikumbua huwa naumia sana,ilikuwa kati ya Tanesco na Yanga uwanja wa Maji Maji Songea ilikuwa baada ya yanga kusawazisha bao kipindi cha kwanza tayari matokeo ubaoni yalisomeka bao 1-1,basi kuna mpira ulipigwa toka winga ya kushoto mabeki wote wa Tanesco waliuzwa mpira ukanaswa na mshambuliaji wa yanga akaachia shuti kali! Mimi nikatema mpira basi wakati naukimbilia kwa mara nyingine wote wawili tukaanguka chini laini mchezaji wa yanga akaniwai na akadokoa mpira kwa mguu ubao ukasomeka yanga 2,sisi 1 hadi mwisho wa mchezo.

Mchazaji Mkali.

“Ramadhani Singano “messi” ananikosha sana ni wachezaji wachache wenye uwezo wa kuingia na mpira eneo 18 bila woga, wachezaji wengi  mara nyingi ni waoga kuingia eneo hilo badala yake hurudisha mpira nyuma.

Ushauri  Taifa Stars &Mbinga

“umakini uwepo katika soka la nchi yetu la sivyo! uwezekano wa kushiriki kombe la dunia ni kuanzi miaka ya 2025 na kuendelea baada ya kuangamia kizazi hiki,kushiriki fainali za kombi la dunia yanaitajika maandalizi ya kweli.

“Baada ya miaka Kadhaa Wilaya ya mbinga itakuwa na timu ligi kuu kwa kuwa uchumi wa Mbinga unaenda kasi sana na mara nyingi wadau wa soka wanakaa vikao kuhusu jinsi ya kuendeleza soka  soka la mbinga,kuna timu kama mbinga united  itafanya vizuri.

Maisha ya sasa.
“Mimi ni mfanyakazi wa Tanesco wilayani Mbinga,pia ni kocha msaidizi wa Mbinga United,umri wangu ni miaka 42, kwa sasa sina mke nina watoto watatu,anaitimisha  Hamis Mtepa ambaye anawakumbuku sana  Iddi Panzi [father],Stivin Nemes [maji Maji] pamoja na Amis Makana [Coastal] ambao walimpa mwanga wa kucheza kwa kujituma.




Chapisha Maoni