Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




ENDELEA KUFUTALIA HISTORIA YA STIVIN MAPUNDA GARRINCHA LEO ANASIMULIA  TUKIO LA KUFUNGIWA NCHINI NIGERIA,PAMOJA NA KURUDI MAJI MAJI AKITOKEA SIMBA

Kurudi Maji Maji.
Displaying mpira 1.jpg
 STIVINI MAPUNDA GARRINCHA ALIYEVAA TSHETI NYEUSI KULIA.


“mwaka 2005 niliamua kurudi maji maji kutokana na migogoro ambayo ilikuwepo ndani ya clabu ya Simba hali ambayo ilipelekea mimi na mwezangu kufungiwa pasipo kujua kosa letu na kututaka kuandika barua kwa kuwa sikuwai gombana na mtu yeyote ndani ya Simba nikaamua kuondoka kwa Moyo mweupe na kurudi  katika timu yangu ya Zamani Maji Maji Fc.

“niliendeleza soka nikiwa na maji maji  toka nilipotoka Simba kwa misimu Kadhaa na baadae nikaamua kutundika daruga na kujishughulisha na shuguli za kawaida.

TULIFUNGIWA SIKU NNE NCHINI NIGERIA

“mwaka 2004 tulifungiwa chumbani siku 4 nchini Nigeria na ubarozi wa Tanzania ili kutunusuru tusikamatwe mara baada ya kuchelewa toka nchini Benin ambako tulitoka kucheza kati yetu na timu ya Taifa  ya Benin mechi ambayo tulifungwa goli 4-0,na mara baada ya kufika Nigeri tulikosa usafiri  baada ya kukuta ndege ambayo tulitakiwa kusafiri nayo  imeondoka na kipindi hicho Tayari visa zetu kusafiria zilikuwa  zimekwisha.

“Barozi wa Tanzania inchi Nigeria SiSiko ilimlazimu kutufungia chumabani huku tukila nyama na kipande kimoja na mkate mara moja kwa siku kama Gerezani kwa uzembe ambao ilifanywa na viongiozi wetu,na hatimaye siku ya 4 tulifanikiwa kuondoka na viongozi wetu hawakuwai kuzungumzia chochote kuhusu tukio lile.

“Inanisikitisha sana kwa timu ya taifa kukwama ugenini kwa kipindi cha siku 4, mimi binafsi kwa kipindi chote cha maisha yangu hapa duniani siwezi kusahau”.alisema mapunda.

Endelea kufuatilia atasimulia ugomvi kati yake na kiongozi wa Fat kipindi kile.


Chapisha Maoni