Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


 
Stivin Mapunda [GARRINCHA] aliyevaa Tsherti nyeusi kulia.

Displaying mpira 1.jpg

Stivini mapunda [Garrincha] ni miongoni wa washambuliji hatari sana ambao wamewai tokea hapa nchini na akafanikiwa kutikisa soka la Tanzania kuanzia mwaka 1997-2005,akichezea timu ya  Maji Maji ya Songea ,Wekundu wa Msimbazi ‘Simba’ na Timu ya Taifa [99-2005]


Displaying mpira 3.jpg
Garrincha alianza kucheza soka toka shule ya msingi Hanga, Darasa la tatu akiwa na miaka 9 na akiwa sekondari alifanikiwa kushiriki michuano mbali mbali ya shule pamoja na Umiseta hadi ngazi ya Taifa ambapo kipaji chake kikaonekana na kuanza kung’ara nchi zima.

katika kipindi hicho akiwa shule ya msingi Garricha alipata nafasi ya kwenda kucheza soka Ulaya kupitia kwa mzungu aliyekuwa kocha wa maji maji wakati huo ambaye alikiona kipaji chake wakati timu hiyo  ilikuwa ikiweka kambi mara kwa mara huko Hanga, lakini baba yake alikataa kutokana na kuofia usalama wa mwanao kwa kuwa  alitaka mwanao asiende mbali nae:-anasimulia….

“Kocha wa maji maji kipindi hicho toka Brugaria alitaka kunichukua ili nikasome ulaya Pamoja na kuendeleza kipaji changu cha Soka baada ya kukiona kipaji changu shuleni Hanga wakati wao walipokuwa wameweka kambi, bahati mbaya baba yangu alikataa kwa kuofia usalama wangu pindi nitakapo kuwa mbali nae hivyo ikashindikana,alisema mapunda.

mwaka 1993 Mapunda alianza kucheza soka la ushindani akiwa na timu ya Taiger mbeya timu ambayo alicheza kwa kujituma sana ambapo kiwango chake kiliongezeka siku hadi siku na mwaka 1997 alitua rasmi katika Timu ya Maji maji maarufu kama wanalizombe toka mkoani Ruvuma.

mapunda alicheza kwa umahili mkubwa akiwa na maji maji ambapo aliiwezesha timu hiyo kuchukua ubingwa wa Tanzania kwa mara ya Tatu mwaka 1998 katika ligi ya muungano na yeye alifunga magori ambayo yaliiwezesha timu ya Maji majikuchukua kombe la ligi ya muungano kwa mara ya tatu.

Garrincha anawataja baadhi ya wachezaji wa kikosi cha wanalizombea ambao  walichukua ubingwa mwaka 1998 ni pamoja na Ivo Mang’itu[marehemu],John Alex,Amri Said, Martin,Stivin Mapunda,Twaa omari[marehemu],Godfrey kikumbizi,Kelvin haule,Said msham[marehemu] pamoja na Omari Husein ambao waliipeleka Maji Maji kwenye michuano ya kimataifa.

Hata hivyo kutokana nyota yake kuendelea kung’ara kwa kiwango cha hali ya juu sana na kusakwa na timu kubwa hapa  nchini  ilimlazimu kuipa kisogo timu yake ya nyumbani na akajiunga na Wekundu wa msimbazi Simba,mwaka 1999,timu ambayo aliichezea kwa mafanikio makubwa sana na aliisaidia timu hiyo kunyakua mataji mbali mbali iiwemo kombe la Tasker,ligi kuu bara, pamoja na kombe la mapinduzi lakini kubwa zaidi alisaidia kuifikisha Simba kwenye robo fainali ya clabu bingwa afrika mara baada ya kuwasambalatisha vigogo wa soka toka  Misri[ Zamareck] kwa mikwaju ya Penalti na kufanikiwa kuingia Robo Fainali.

Safari yao katika ligi ya mabingwa iliishia Robo fainali mara baada ya kuchezea kipigo toka kwa Mabingwa wa Ivory [Isec Mimosas] katika mechi ya marudiano ambayo Simba walichezea Ugenini na hatimaye wakaaga Rasmi mashindano..............................


usikose kufuatilia makala hii ya Stivin Mapunda ataendelea kusimulia mengi kuhusu historia yake ya soka ikiwemo Tukio la kufungiwa siku nne nchini Nigeria AKIWA NA TAIFA STAR.


Chapisha Maoni