Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


 TAREHE 10-04-2014.
Na S ophia Mwaipyana,Mbeya.

Displaying KALINGA 2.jpg
 Ukiwazungumzia wanawake wapiganaji katika soka nchini Tanzania basi huta sita kumtaja  Elizabeth Kalinga aliyejikita katika soka akiwa ndiye  mwamuzi katika mpira wa miguu.

 Elizabeth huyu ndiye mwamuzi wa kwanza  mwanamke katika nchi yetu aliyefanya kazi hii ya uamuzi   kwa kipindi kirefu akiwa kama  mwanamke, amejizolea umaarufu mkubwa kwa kuwa ni wanawake wachache wamefanikiwa kuhimili kufanya kazi katika sekta ya michezo.
 
Lakini kwa mwanamke huyu aliye jaa ujasiri mkubwa  yeye hakuamini  kauli iliyo kuwa  imetawala katika jamii nyingi za kitanzania ambayo ilimwona mwanamke hawezi kitu na walikuwa wakibaguliwa sana katika sekta mbalimbali.

Mwanamke huyu shujaa alijikita katika kazi ya uamuzi na alikubalika sana kwa utendaji wake mzuri wa kazi yake japo wengi walimchukia kuona akiwazidi kiwango cha uamuzi kwani mwanadada huyu alikuwa na uwezo mkubwa sana katika kazi hii ya uamuzi.

 Ulianza lini kazi hii ya uamuzi?
 
Nilianza kujifunza kazi hii ya uamuzi mwaka 1980 mafunzo hayo niliyachukulia nchini Zambia na ndani ya mwaka huu nilianza kuchezesha ligi daraja la tatu.
 
“nilikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuchezesha soka hata kuwashinda wanaume ilifika kipindi nilikuwa nikipangiwa kuchezesha mechi ngumu zote nilikuwa nikipangiwa mimi kwa kujua kuwa ninauwezo mkubwa wa kuchezesha mchezo bila upendeleo”

Mechi gani ilikuwa ngumu kwako?
 
“sikumbuki mwaka lakini hii ndiyo ilikuwa mechi ngumu sana kwangu ilikuwa ni katika ya timu ya Yanga na Mirambo siku zote timu ya Mirambo walikuwa wakorofi sana”
 
“lakini kwangu walijikuta wakiwa wapole kutokana nilichezesha ile mechi bila upendeleo palipo kuwa panastahiri kutoa adhabu nilitowa bila  kujali huyu ni mchezaji wa timu gani”
 
Changamoto gani ulizo kuwa ukikutana nazo katika kazi yako.
 
“kama unavyojuwa kipindi kile watu walikuwa wanamwona mwanamke hawezi kitu hivyo walikuwa wana nidharau lakini nashukuru mungu walikuwa wananiheshimu”
 
“pia mechi nyingi ngumu nilikuwa napewa nichezeshe mimi walikuwa wakihisi  nitashindwa, kunawakati walifanya mambo kwa kunikomoa kwani kuna baadhi ya makocha na viongozi walianza kunichukia baada ya kuona nawazidi umahili kwani ilifika wakati jamii ilinikubali sana“
 
Vipi kuhusu rushwa kwa waamuzi.
 

“kiukweli vishawishi vipo lakini swala la kupokea au kukataa ni  uamzi wa mtu na kumbuka kunamechi moja  sikumbuki mwaka viongozi wa timu Fulani walimpa msaidizi wangu rushwa aje anipe mimi”
 
“alipoleta nilimwambia kaanazo mchezo ulipo malizika wale viongozi  wakanifwata  wakiniuliza kwanini tumekupa pesa halafu timu yetu haujaifanyia msaada  uwanjani nikawauliza mlinikabidhi mimi hizo pesa?, kwahiyo vishawishi nivingi ila mwamuzi yeye mwenye ndiye anatakiwa kuwa na msimamo”
 
kazi hii ina ugumu gani?.
 
“kazi hii haina ugumu wowote  ilimradi  uzijuwe sheria  na kufanya mazoezi kila wakati ila ukiwa mvivu  ndipo kazi hii huwa ngumu”
 
Nini utofauti wa waamuzi wa sasa na zamani
 
“waamuzi wa  zamani tulikuwa  hatuwezeshwi, tunajitegemea vifaa vya michezo pia tulikuwa tukipewa nauli  peke ,lakini waamuzi wa sasa wanawezeshwa”
 
“pia wamuzi wa zamani walikuwa wakipewa kazi hii ikiwa unakazi nyingine walikuwa wakihofia iwapo mtu akipewa hana kazi nyingine walihofia ata shawishika na kupokea rushwa”
 
Tukio gani ambalo huwa haulisahau
 
“kitu ambacho huwa hakinitoki katika kumbukumbu zangu ni katika ya mwaka 2000 au 2001 nilipolipwa shilingi 5000 tu baada ya kuchezesha mechi ya Mtibwa na Prison ambayo walichezea Morogoro”
 
“pesa hiyo nilipewa ikiwa ni garama zote za mchezo hivi vilikuwa ni visa kwa viongozi  ambao walitaka niipendele timu yao kwakuwa walikuwa nyumbani,iliniadhimu nitumie pesa zangu mwenyewe kurudi nyumbani Mbeya”
 
Jamii ilikuwa inakuchukuliaje
 
“kiukweli kwa miaka ile watu wengi walikuwa wana niona kama muhuni flani na msichana wa ajabu sana kulingana na utamaduni wetu wa kitanzania mtoto wa kike walikuwa  wakimdharau sana”
 
Unalionaje soka la mkoa wa Mbeya kwa sasa.
 
“katika mikoa iliyo jaliwa Baraka ya vipaji vingi katika soka basi mbeya ni moja wapo,soka linazidi kukuwa kwani mkoa sasa una timu mbili ligi kuu na moja ligi daraja la kwanza hivyo maendeleo ni makubwa sana na wadau wazidi kuzisapoti timu zote

Uashauri wako kwa vijana pamoja na wachezaji
 
“wachezaji  wajitume kwa bidii iliwajitangaze huku waki zingatia nidhamu na mafunzo wanayo fundishwa na walimu wao iliwawezesha kuwa wachezaji wa kimataifa”
 
“kwani kupitia mpira tunapunguza tatizo la ajira kwa vijana na tunaweza kuondoa umasikini kwani mpira nikazi kama kazi nyingine”
 
Katika familia yenu nani amefuata nyayo zako?.
 
“hapana ila alikuwepo mdogo wangu ambaye nilimfundisha ubondia lakini kwa bahati mbaya alifariki,lakini yupo mjukuu wangu ambaye anapenda sana  kazi kama yangu naimani Yule atarithi mikoba yangu”

Baada ya kuachana na soka mwaka 2002
 
Displaying REFA.jpg
 
 
 
 
 
 
 
 Kwasasa ni mtendaji wakata ya Ruanda na katibu tarafa wa kata hiyo ,lakini katika  soka ni mwenyekiti wa soka la wanawake mkoa”
 
 
Soka la wanawake katika mkoa wetu lipo vipi.
 
“kuna watoto wenye vipaji vizuri hivyo wazazi na wadau wasoka tunawaomba wazidi kuwapa sapoti watoto wakike kwani nao wana weza”



Chapisha Maoni