Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Sehemu ya mwisho ya historia ya maisha ya soka ya Kelvin Yondani mzaliwa wa mwanza ambaye alicheza simba na reli ya morogoro kiboko ya vigogo.
 ilipoishia,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
“Basi kutokana na tuuma ile na licha ya kwamba kiwango changu kilikuwa kikubwa masikini ya mungu sikupewa nafasi hata ya kusafiri na timu kwenda nchini Msumbiji katika mechi ya marudiano waliniacha Bongo.

“Kuanzi hapo nilichukiwa sana hadi nikahasirika kisaikorojia pindi nikiwapo uwanjani lakini ukweli ni kwamba mimi sikuwa na mapenzi na Yanga na kukosa Bao ni suala la kawaidi kwa mchezaji sio makusudi.

songa nayo

Waamzi.

“Viwango vyao vipo chini sana hawjiamini pindi wawapo uwanjani kutokana na  kupokea Takribani toka pande mbili hali hiyo inapelekea wachezaji kuchezeana rafu mbaya na mwamzi anajifanya haoni.


“Mfano kuna tukio lilitokea Hivi karibuni la Haruna Moshi Boban kumchezea Rafu mbaya Kelvin Yondani [Yanga]mwamzi badala ya kutoa kadi nyekundu akatoa kadi ya njano huu ni uzembe mkubwa kwa waamzi wetu lazima wabadilike.


Katiba.

“TFF lazima wafanyie mabadiliko ya katiba ya soka hapa nchini hasa kipengere cha uchaguzi badala ya wanachama wachache kumchagua kiongozi wa chama wa ngazi ya chini au ya juu badala yake achaguliwe na umaa, ili kuepuka tatizo la watu wachache wenye pesa wasiojua mpira kuchukua madarada kwa kuwaonga wapiga kura.


“Kuna kipindi nilijisikia aibu sana wakati nilipoenguliwa mwaka 2005 katika nafasi ya ujumbe Ilemela na wakampa mtu kutokana na vijiela vyake ambaye hajue chochote kuhusu mpira kunishinda mimi.

Wachezaji anaowakubali

“Namkubali sana Haruna Niyonzima kiungo wa Dar Es Salam Yang Afrika yupo Vizuri kwa ukanda huu wa afrika mashariki na kati, lakini sio kwamba napendelea ni ukweli ni Mtoto wa kaka yangu Kelvini Yondan Anafanya vizuri katika nafasi ya Ulinzi kwa hivi sasa hapa nchini.

Kipa Msumbufu.

“Mwameja huyu ni balaa mimi nadiriki kusema kuwa hakuna mlinda mlango ambaye hadi hii leo amefikia uwezo wa Mwameja.

“Mimi alikuwa akinisumbua sana ,mara nyingi mazoezini alikuwa anawaita na kuwawekea mpira eneo la penalti na kuwaambia atakayefunga penalti tano nampa fedha,lakini matokeo yake unaishia tatu au mbili,mimi sikuwai shuhudia Mwameja akifungwa Penalti 5.

Ushauri kwa Timu ya Taifa.

“Hata ashuke Yesu, kwa mfumo wanaoutumia Taifa Stars na haina ya wachezaji walionao kushiriki kombe la dunia ni ndoto,lazima yafanyike mabadiliko makubwa sana ili kunusuru soka letu.

“Mimi kipindi nacheza nilikuwa na nguvu sana hizo nguvu za Thomas Ulimwengu ambaye ni nchezaji mwenye nguvu kwa kipindi hiki hata robo kwangu hatii ndani,wachezaji wa kipindi chetu  walikuwa na vitu vingi sana ni mchezaji gani? Wa sasa ivi ana uwezo wa kumwamisha beki kwenye Reli na kupasia wavu,hakuna.

“wachezaji  wenye vipaji vya kweli tunawacha na badala yake tunawakumbatia wachezaji wasio na akiri ya uwanjani,Tff wanakijua cha kufanya.


Baada ya kustaafu.

“Kwa sasa nina miaka 48,nina mke na watoto wawili ,najisughulisha na ufugaji wa ng’ombe wa Maziwa pamoja udalali wa kutafuta Bidhaa Mbali mbali Zinazopatikana hapa Mwanza kwenda Dar  na mke wangu ajishughulisha na ufugaji wa Kuku wa kisasa maisha yetu Sio mabaya.

“kwa kweli sikunufaika na mpira kiuchumi ila kuwa maarufu na kufahamiana na watu imenisaidia sana kufanya shughuli zangu kwa uraisi,Anahitimisha Yondani ambaye ametokea katika ukoo wa wachezaji wa ukweli wa soka na watoto wake muda wote anawahamasisha kuhusu mpira,na wanacheza vizuri.


Chapisha Maoni