Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




 
Sophia Mwaipyana,Mbeya
 
Timu ya kimondo Sc ya wilayani mbozi mkoani hapa  inayoshiriki ligi daraja la kwanza  imewataja wachezaji  15 ambao wataendelea kuitumikia timu hiyo na wachezaji walio watema  katika kikosi hicho .

Akizungumza na Championi Juma tatu  katibu msaidizi wa timu hiyo Silla Yalonde amesema wameamua kubakiza wachezaji 15 na watasajiri wengine ambao watajulikana hapo baadaye baada  usajiri kukamilika  hii ni kutokana na pendekezo la benchi la ufundi ambalo linahitaji kikosi kidogo cha watu wachache lakini chenye ufanisi mkubwa kwani wanajipanga vizuri kwaajili ya kupanda ligi kuu.

Yalonde amewataja wachezaji hao kuwa ni Azishi Saimoni Petro,Emamanuel OthmanChacha,Meshack Simbeye, Baraka Mtafya,Casmir Frank Mwamboka,Mashaka David Mwakyoma,,Job Sichone,Issa Kapweka,Asifiwe Lwinga, Geofrey Mwashiuya,Bright Berbatov Sichalwe,Mwamba Mkumbwa,Geofrey Mine Mlawa,Joshua Omary Ally na Patrick Mangungulu.

Aidha amewataja wachezaji walioachwa na timu hiyo kwa sababu mbalimbali ikiwemo kwenda masomoni, kushuka viwango na kumaliza mikataba yao kuwa ni Ramadhani Hussein Sangai, Twaha Zubeiry Mageha,Daudi Martin Mwaipyana, Guna Benedict Miho, Patrick Mwitilila Mwamengo, Rodgers Mwaisoloka,Joel Kasimila,Abu Suwilanji Mwamengo,Afrika Junior Simbeye, Daudi Mafufu Mwanja, John Mwanji,Charles Hizza, Christopher Kassewa,Sille Sanga,na Amirson Mohamed Bori.
 
 Pia ameongeza kuwa wachezaji walibaki katika timu wameanza kambi leo na ambao hawaja fika wametakiwa kuingia kambini kwaajili ya kuanza mazoezi na kocha ili wajipange vizuri kwa msimu ujao.

 Amewataka wadau wa soka kujitokeza kwa wingi kuisapoti timu hiyo ikiwa ni pamoja na kuiombea timu hiyo ifanye vizuri pia kufadhiri timu hiyo kwa hali na mali pia mawazo ili timu hiyo iweze kupanda daraja na kushirikiligi kuul.


Chapisha Maoni