Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





???????????????????????????
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI, BLOGU NA TOVUTI (16.07.2014)
Historia ya Klabu ya Simba Tangu 1920 hadi 2014
Mwandishi: Mwina Kaduguda
Mchapishaji: Mkuki na Nyota Publishers
Mwaka: 2014
Kurasa: 128
Bei: Shilingi 15,000/= 
Muhtasari wa Kitabu
Hiki ni kitabu cha kwanza chenye historia ya kina ya Simba Sports Club. Kama mpenzi wa soka, hususan mkereketwa wa Simba, utajua chimbuko na undani wake tangu ilipoanzishwa hadi hii leo. Vilevile utaweza kutumia kitabu hiki kama ushahidi katika mabishano na mijadala inayohusiana na klabu, wachezaji, viongozi, timu pinzani na bila kusahau historia ya soka la Tanzania kwa ujumla.
Utasoma vioja vya soka letu kama vile ushabiki wa kupindukia, vituko na imani za kishirikina, makundi yaliyotia fora, migogoro, mafanikio, picha za matukio mbalimbali, bila kusahau rekodi za mwenendo wa timu na misimamo ya ligi katika historia ya klabu.
Kwa kukisoma kitabu hiki utafahamu pia mambo mengi yanayolizunguka soka la Tanzania, kwani rekodi hizi hazipatikani kwa urahisi na mwandishi ametumia muda mwingi kufanya utafiti na kukusanya taarifa kutoka vyanzo mbalimbali rasmi kama vile maktaba, vitabu, magazeti, nyaraka na kuwahoji wazee wa zamani. Kwa mfano, utajua ni lini soka liliingia na kusambaa nchini katika karne ya 20, mpasuko uliozaa Simba na Yanga na mengine mengi ya kuburudisha, kuelimisha na kusisimua.
 Kuhusu Mwandishi
Mwina Mohamed Seif Kaduguda, mzaliwa wa Kasulu, Mkoa wa Kigoma ana shahada ya Bachelor of Arts (B.A. Hons), Ushirikiano wa Kimataifa na Utawala, UDSM 1992, Cheti cha Uandishi wa Habari-TSJ, 1994. Ana Diploma ya Ukocha wa Soka HUPE-Budapest, Hungary 1997, Cheti cha Utawala wa michezo-IOC, 2001, Cheti Cha Uamuzi wa Soka-FRAT, 2001 na Cheti Cha Juu cha Ukocha-CAF, 2006.
Ameshika nafasi nyingi za uongozi wa Mpira wa Miguu nchini zikiwamo zile za Katibu Mkuu FAT sasa TFF, 2003–2004, Katibu Mkuu TAFCA, 2002–2008, Katibu Mtendaji SPUTANZA, 2001–2004, Katibu Mkuu TASWA, 1997–2004 Mkufunzi Msaidizi wa Makocha wa soka TFF, 2006, Katibu Mkuu SIMBA S.C., 2006–2010 na Mjumbe BMT, 2000–2005. Ameshiriki katika makongamano ya kimataifa ya michezo Toronto-Canada, Athens-Ugiriki, Kuala Lumpur-Malaysia na Sandton City-Afrika ya Kusini.
Hivi sasa ni mwalimu katika Shule ya Sekondari ya Jitegemee, Dar es Salaam na anapatikana kwa mahojiano na majadiliano kuhusu mada mbalimbali zilizomo kitabuni. 
KWA TAARIFA ZAIDI AU MANUNUZI YA JUMLA NA REJA REJA WASILIANA NA:
Mkuki na Nyota Publishers Ltd
Simu: 0787558448
24, Samora Ave, Dar es salaam. 
TPH Bookshop (Dar es Salaam)
Simu: 0687238126
24, Samora Ave, Dar es salaam. 
TPH Bookshop (Dodoma)
Tel: 0783446790
Gorofa ya Pili, Jengo la Chimwaga, UDOM–Dodoma
Pia kinapatikana katika maduka ya vitabu na stendi za magazeti mbalimbali nchini. Pata nakala yako sasa! Bei ya rejareja ni Shilingi 15,000/= tu


Chapisha Maoni