Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Timu ya soka ya maji maji toka mkoani Ruvuma imesajili wachezaji wapya sita wakiwemo wawili toka kwa wapinzani wao Mlale JKT ili kuimarisha kikosi chao kabla ya michuano ya ligi Daraja la kwanza kuanza kutimua vumbi kwa nchini zima.

Wachezaji ambao wamesajiliwa toka Jkt Mlale ni Mkongwe aliyepata kuweka hapa nchini Kudra omari pamoja na Idd Kipagwile,wachezaji wengine waliosajiliwa toka nje ya mkoa wa Ruvuma ni Ally Hassan,David Abdallah,Yusuph mgwao pamoja naSaid zeco ambapo wataongezez nguvu kikosi hicho.
Akizungumza na championi Ijumaa Meneja wa timu hiyo Good Mvula alisema kikosi hicho kitaingia kambini,jumatatu mjini songea kabla ya kambi hiyo kuamishia katika mji mdogo wa peramiho,na lengo kubwa ni kuwa na kikosi imara ambacho kitawawezesha kupanda daraja msimu huu.

“maji maji tunaitaji kupanda daraja vyovyote itakavyokuwa tumesajili wachezaji 6,na bado tupo mawindoni kuwanasa wachezaji wengine wakubwa kutoka katika vilabu vikubwa hapa nchini,tunaomba wanaruvuma wote watuunge mkono,alisema mvula.

Mabingwa hao mara 3 wa kombe la muungano walianza kuyumba toka miaka ya 2000 ambapo adi kufikia hii leo wameshingwa kuimili mikikimikiki licha ya kupanda ligi kuu mara kadhaa.


Chapisha Maoni