Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




Niliishi maisha magumu Msimbazi mara bada ya kukosa bao la wazi dakika za mwisho mechi ya kimataifa dhidi ya timu toka msumbiji CCM Kirumba Mwanza. kwa wachezaji tulionao hivi sasa na mfumo wa uendeshaji wa timu ya taifa, hata kama atashuka Yesu kushiriki kombe la dunia ni ndoto.


.


MBUI YONDANI.


 Mbui Yondani ni miongoni mwa washambuliaji wapiga mashuti hatari sana ambao waliwahi tokea hapa nchini na kamwe hawezi kusahaurika kwa mashabiki na wadau wa soka hapa nchini hasa kwa Timu ambayo zamani ilikuwa kiboko ya vigogo hapa nchini nazunguzia  Reli Morogoro .

 Yondani ambaye ni mzaliwa wa mtaa wa Kirumba Polisi Jijini Mwanza ambaye ni Baba yake mdogo wa Beki  mahili wa Yanga Kelvin Yondani, alianza kusakata kabumbu wakati akiwa mdogo katika shule ya Msingi mwenge iliyopo Jijini Humo.


 Katika Mazungumzo maalum na JELAMBA VIWANJANI ameeleza kwa kina kuhusu historia yake ya soka;

 “Licha ya kucheza mpira katika timu ya Uwanja CCM Kirumba pamoja na Basuko,nilianza kucheza soka la ushindani mwaka 1988 katika timu ya Copy United ambayo ni timu ya watoto wa mjini Mwanza timu ambayo wamepitia wanasoka wengi wa mkoani Mwanza.


“Mwaka 1989 nilijiunga na Reli ya Morogoro timu ambayo ilikuwa tishio kwa vigogo hapa nchini nazungumzia Simba na Yanga,wakati nipo Reli nilipata nafasi ya kuchezea timu ya Taifa kwa mara ya kwanza mwaka 1992 kutokana na kiwango changu kuwa juu sana kwa kipindi hicho,nakumbuka tulicheza kwenye michuano ya Challenge  ambapo Tanzania tuliwakilishwa na Kaka Kuona pamoja na Victoria,Hayo ni majina ya timu ya Taifa Sisi tuliwakilishwa na timu mbili kwa kuwa tulikuwa waandaaji .

 “Baada ya kupata nafasi ya kuitumikia Timu ya Taifa mwaka 1993 nikasajiliwa na Simba  ya Jijini Dar Es Salam,Timu ambayo niliichezea kwa msimu mmoja lakini kutokana  na mizengwe,kocha alikuwa anawapanga wachezaji kulingana na mapenzi yake hata kama wewe ni mzuri,Na ni ukweli usiopingika kipindi kile  nilikuwa mchezaji wa kiwango cha juu sana,


 “Baada ya kuona kwamba Simba naweza nikaua kiwango changu  mwaka 1994 nikatimukia Milambo ya Tabora,lakini kutokana na maisha magumu ya huko Tabora,Timu yangu ya Zamani Reli ya Morogoro wakaamua kunirudisha, hapo nilicheza kwa miaka miwili 1996 hadi 1998.



“Mwaka 1998 hapo nilifikia juu ya kustaafu soka  na kuangaika kuhusu  maisha yangu kwa kuwa kwa kipindi chote hicho sikuwa vizuri kiuchumi, nikaacha kucheza Soka la ushindani nikachezea Mwanza Veterani Pamoja na Pamba ya mwanza ambapo Mwaka 2002 nikaacha kabisa kujihusisha na Mambo ya soka hapo ndipo nikatundika Daruga Rasmi.



Nakumbuka.



“mwaka 1990 wakati nipo Reli ya Morogoro tulicheza na Timu ya soka ya Maji Maji ya Songea,katika pambano hilo ambalo lilikuwa kali sana kutokana na Maji Maji kuwa na kikosi imara hadi kipindi cha kwanza kilipomalizika nakumbuka tulifungana bao 1-1,



“Kipindi cha pili mchezo ulianza kwa kasi sana ambapo dakika za mwisho nilipokea Pasi safi nje ya 18 na bila kufanya ajizi nilifumua Shuti kali ambalo lilipeleke mlinda mlango wa Maji Maji kuchanika mikono na kuachia mpira ukaingia Wavuni.





“Mimi mwenyewe nilishangaa sana tukio lile mara baada ya kumkuta bwana Shaibu Kambanga Disko usiku baada ya mechi akiwa amefungwa bendeji,nikampa pole na akanieleza kuwa hakuwai pata mkwaju kama ule,tukaendelea kuburudika.



“Nakikumbuka kikosi cha Reli ambacho kilikuwa kiboko ya Vigogo na Timu zingine hapa nchini,ambacho akitakuja sahaurika hapa nchini ambapo langoni alikuwepo Athumani Msumari,safu ya ulinzi iliimalishwa na  James Charles[marehemu],Abdallah  Mkali[marehemu],Gasper Lupindo[marehemu] pamoja na Fikiri Magoso. Viungo alikuwepo Mtwah Kiwelu,Boniface Njohore pamoja na Dankani Butinini huku safu ya ushambuliaji ikiongozwa na mimi mwenyewe  Mbui Yondani,Msafiri Khamis Bila kumsahau Living Stone.





Hawaezi kusahau



“Mwaka 1991 mechi ya ligi kuu kati ya Reli na Bandari ya Mtwara mimi na beki wa Bandari tuliruka juu kuuania mpira mara baada ya kuingizwa majaro zuri toka winga ya kulia bahati mbaya tukaukosa mpira na tukagongana Vichwa na tukadondoka vibaya sana.





“Katika tukio lile mwenzangu alipata fahamu baada ya siku ya Tatu,mimi japokuwa nilirudi uwanjani kuendelea na mchezo usiku uliofuata sikupata usingizi nilipata maumivu ambayo sikuwai kuyapata tangu nilipozaliwa kwa Baba na Mama, ambapo baada ya siku chache niliendelea na mchezo.

 Endelea kusoma jelamba viwanjani sehemu ya pili atasimulia kuhusu imani za kishirikina pamoja kubebeshwa gunia la misumari na samba usikose.


Chapisha Maoni