Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




 ENDELEA KUFUATILIA HISTORIA YA MBUYI YONDANI BABA MDOGO NA KELVIN YONDANI MCHEZAJI WA SASA WA YANGA.

.
ILIPOISHIA JANA……………………..
“Mwaka 1991 mechi ya ligi kuu kati ya Reli na Bandari ya Mtwara mimi na beki wa Bandari tuliruka juu kuuania mpira mara baada ya kuingizwa majaro zuri toka winga ya kulia bahati mbaya tukaukosa mpira na tukagongana Vichwa na tukadondoka vibaya sana.


“Katika tukio lile mwenzangu alipata fahamu baada ya siku ya Tatu,mimi japokuwa nilirudi uwanjani kuendelea na mchezo usiku uliofuata sikupata usingizi nilipata maumivu ambayo sikuwai kuyapata tangu nilipozaliwa kwa Baba na Mama, ambapo baada ya siku chache niliendelea na mchezo.
ENDELEA………………

Ushirikina

“Upo hasa kwa virabu vikubwa Simba na Yanga mara nyingi hasa katika mechi za watani wa jadi lakini kwa timu zingine kama Reli sikushuhudia suala lolote la ushirikina tulikuwa tunafanya mazoezi na kumtegemea mungu.
“Siamini hata kido imani hizo sio kweli ,wakati nipo  Simba kuna mambo mengi yalikuwa yanafanyika wakati wa mchezo lakini tulikuwa tukichezea kichapo kama kawaida.


Simba walinibebesha Gunia la Misumari.

“Mwaka 1993 wakati nikiwa Simba,nilikosa bao Ya wazi wakati zikiwa zimesalia dakika 3 mpira kumalizika,katika kombe la Caf kwa sasa shirikisho,kati ya Simba na Timu Toka Msumbiji,nakumbuka ilikuwa CCM Kirumba Mwanza mchezo ambao ulimalizika kwa sare ya bila kufungana.



“Baada ya mechi ile sikuwa na amani,wenye timu walinitazana kwa jicho baya  huku wakinituhumu kuwa mimi ni mpenzi wa Yanga na kwamakusudi nikaamua kuwakosesha Simba ushindi kiukweli iliniuma sana.


“Basi kutokana na tuuma ile na licha ya kwamba kiwango changu kilikuwa kikubwa masikini ya mungu sikupewa nafasi hata ya kusafiri na timu kwenda nchini Msumbiji katika mechi ya marudiano waliniacha Bongo.

“Kuanzi hapo nilichukiwa sana hadi nikhathirika kisaikorojia pindi nikiwapo uwanjani lakini ukweli ni kwamba mimi sikuwa na mapenzi na Yanga na kukosa Bao ni suala la kawaida kwa mchezaji sio makusudi.

  Endelea kusoma jelamba viwanjani sehemu ya tatu kuhusu waamuzi,katiba  na kipa ambaye alimsumua sana usikose.


Chapisha Maoni