Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Na Alex Mapunda,Iringa

KUELEKEA uchaguzi wa viongozi wapya katika timu  ya soka ya Lipuli mkoani Iringa Tayari kamati ya uchaguzi imeshachuja majina ya wagombea na yameshabandikwa katika mbao za matangazo.

 Akizungumza na JELAMBA VIWANJANI  mwenyekiti wa uchaguzi wa timu hiyo Jackson Ibrahim Chaula  alisema kati ya wagombea  9 ambao waligombea katika nafsi mbali mbali  jina  ambalo ilienguliwa ni  la Daudi masasi baada ya kutokidhi vigezo ikiwemo kukosa cheti cha kidato cha nne pia aliwakata wagombea kuanza kampeni siku tatu kabla kama zisemavyo kanuni na taratibu za timu hiyo.

“uchaguzi ni tarehe 28,maandalizi yanaendelea vizuri kikubwa ni kila mgombea kutii taratibu na kanuni za uchaguzi,ambapo kampeni ni siku tatu kabla ya uchaguzi ambaye atakiuka hatua kali zitachukuliwa  dhidi yake”alisema chaula.

Chaula aliongeza kuwa wanachama wa Lipuli wanatakiwa kujitokeza kwa wingi  wakiwa na kadi zao ili kumchagua kiongozi ambaye ataiongoza timu hiyo kwa ufanisi mkubwa  na ikumbukwe kuwa makosa  watakayofanyika yatawaghalimu wanairinga kwa miaka 4. 

Awali  uchaguzi huo ulitakiwa kufanyika  tarehe 28 mwenzi wa nane lakini wasimamizi waliamua kuahirisha kwa kuwa maandalizi hayakukamirika kwa wakati na mwenzi huu wamejipanga vilivyo ili kuhakikisha uchaguzi huo unakamirika kwa kuwapata viongozi wenye sifa.


Chapisha Maoni