Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Na Alex Mapunda,Iringa
Kocha wa simba Patrick Phiri akiwa na wachezaji wake, wakipasha katika uwanja wa samora.

LICHA ya uwanja wa Samora kuwa uwanja wa michezo na burudani,Kaimu katibu mkuu wa chama cha soka mkoa wa Iringa John Mwakarobo amewatakaa wameriki wa uwanja huo kuzuia baadhi ya shurughuli za burudani kufanyika katika uwanja huo ili kurinda na kutuza miundombinu ya uwanja huo.
Akizungumza na Jelamba viwanjani mwakarobo alisema,miundombinu ya  uwanja wa Samora  inazidi kuwa hatarini ikiwemo pichi ya kuchezea kutokana na shughuli za kiburudani na zingine za kijamii zinazopelekea kujaza watu wengi huwanjani hapo.

“kuna baadhi ya shughuri kama Fiesta pamoja na Mtikisiko ni shughuli ambazo zinazalisha uchafu mwingi katika uwanja wa samora,pia shughuli ambazo zinasababisha kuwepo kwa mashomo katikati ya uwanja,nawaomba wamiriki wa uwanja huo kufanya maamuzi mazuri ambayo yatapelekea kuinusuru hali ya uwanja wa samora.

Pia mwakarobo aliongongeza kuwa wamiriki wa uwanja huo wanatakiwa kushirikiana bega kwa bega na uongozi wa chama cha soka pamoja na wadau wa michezo mkoani hapa ili kuhakikisha wanatatua matatizo sugu ya uwanja huo ikiwemo,tatizo la uzio,pichi ya kuchezea pamoja na mapungufu mengine yote ya uwanja huo ambapo kama Lipuli watapanda daraja msimu ujao wawe na sehemu zuri ya kuchezea.

Lipuli ambayo inatumia uwanja wa Samora kama uwanja wake wa nyumbani wmemaliza katika nafsi ya tatu mzunguko wa kwanza ligi daraja la  kwanza ambapo kama watafanya vizuri mzunguko wa pili wananafasi kubwa ya kupanda daraja msimu huu.


Chapisha Maoni