Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Na Alex Mapunda,Iringa
 IRINGA
TIMU ya soka ya Lipuli ya Iringa Inatarajia kuingia kambini rasmi  maeneo ya veta Iringa Mjini ili kujiwinda na mzunguko wa pili wa ligi daraja la kwanza inayotaraijia kukata utepe hivi karibuni.

Baadhi ya wachezaji wanaotokea dar tayari walikuwa kambini jijini Dar es salam eneo la karume na wanataraji kuwasili mkoani Iringa ili kuungana na wezao toka maeneo tofauti pamoja na wachezaji wapya waliosalijiliwa msimu huu kwaajili ya kambi ya pamoja.

“tumesajili wachezaji wapya watano ambao wataziba mapengo yaliyojitokeza msimu uliopita kama Ripoti ya mwalimu ilivyokuwa ikijieleza,leo jumatano wachezaji wote wanaanza kambi rasmi na maandalizi yote yanaenda vizuri sana”,Alisema Ronjino Malambo.

Vile vile ronjino malambo aliwapongeza wadau na mashiki mkoani hapa kwa sapoti kubwa mbayo wanaitoa kwa timu ya Lipuli ambapo amewaomba waendelee kuiunga mkono zaidi timu hiyo kwa manufaa ya wanairinga wote.

Lipuli inanafsi kubwa ya kupanda daraja msimu huu kama wanadau,mashabiki pamoja viongozi watakuwa kitu kimoja katika kuijenga Ripuli.


Chapisha Maoni