Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.




 
Mechi ya Nani Mtani Jembe namba 2 itafanyika kesho siku ya jumamosi katika dimba la Uwanja ambapo itawakutanisha Young Africans Sports Club dhidi ya Simba SC huku timu  zote zikitarajiwa kuwatumia wachezai wao wapya zilizowasajili katika kipindi cha dirisha dogo.
Kikosi cha mbrazil Marcio Maximo tayari kimeshawasajili wachezaji wawili kiungo Emerson de Oliveira kutoka nchini Brazil na mshambuliaji mkongwe na mzoefu wa hali ya juu Danny Mrwanda ambao wanatajiwa kuongeza nguvu katika mchezo huo wa kesho.
Young Africans chini ya kocha mkuu Marcio Maximo inaendelea na mazoezi katika Uwanja wa Boko Veterani  huku wachezaji wote 26 waliongia kambini wakiendelea kujifua kuwa fit kwa ajili ya mchezo huo wa siku ya jumamosi.
Huu ni mchezo wa pili wa Nani Mtani Jembe kuzikutanisha timu hizi kwani katika mchezo wa awali uliofanyika mwaka jana, Young Africans ilipoteza kwa mabao 3- 1, na kocha Maximo pamoja na wachezaji wake wamejiandaa kuhakikisha safari hii wanapata ushindi kwenye mchezo huo.
Kocha Maximo amesema vijana wake wote wapo kwenye hali nzuri kuelekea mchezo huo, ambapo mchezaji pekee majeruhi ni Jerson Tegete ambaye alipata majeraha hayo katika mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Vipers kutoka nchini Uganda.
 
 Kwa upande mwingine  Habari nzuri kwa mashabiki wa Simba, kiungo mkabaji wa timu hiyo, Jonas Mkude, ameanza mazoezi baada ya kupona malaria iliyomuweka nje ya uwanja kwa wiki moja kwa ajili ya matibabu.


Kiungo huyo alishindwa kumalizia mazoezi ya wiki iliyopita kwenye Uwanja wa TCC, Chang’ombe jijini Dar es Salaam baada ya kutapika kabla ya kufanyiwa vipimo na kukutwa na malaria na kuanza dozi.

Katika mazoezi ya jana yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Chuo cha Ualimu hapa Unguja, Zanzibar kiungo huyo alionekana akianza mazoezi mepesi ya binafsi kukimbia akiwa chini ya uangalizi wa daktari, Yassin Gembe.

Gembe alisema Mkude amepona kabisa na mechi ya kesho Jumamosi ya Nani Mtani Jembe dhidi ya Yanga atakuwepo uwanjani kama kocha ataamua kumtumia.

“Mkude kama unavyomuona hii leo (jana) asubuhi ameanza mazoezi mepesi ya binafsi kwa ajili ya kurudisha afya yake ya kawaida, ameanza mazoezi mepesi na baadaye akafanya ya nguvu pamoja na wenzake.

“Ametokea kwenye malaria, hivyo ni lazima aanzie na mazoezi mepesi ili hali ya kawaida irejee, kocha akiamua kumtumia ni ruksa. Tofauti na Mkude hakuna majeruhi mwingine,” alisema Gembe.

 WEKUNDU HAO



Chapisha Maoni