Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


NA Alex Mapunda,Iringa

BONDIA toka songea  maarufu kwa jina la dume la Simba anatarajia kupanda ulingoni kupambana na Benki mwakalebera katika pambano la raundi 8 litakalopigwa njombe Tarehe 7 siku ya jumapili.

Katika pambano hilo ambalo linatarajia kuwa na upinzani mkubwa pia kutakuwepo na mpambano ya utangulizi ambapo Bondia Alex kiwawa atamenyana na Daudi Joseph Toka Morogoro,Ally Bobu wa njombe atapambana na Furaha Mapepe kisha Poul mavisu wa Songea atavaana na Damas toka njombe.

Akizungumza na JELAMBA VIWANJANI mwalimu  Simba la Dume toka Songea Musa Omari alisema wapo kwenye maandalizi mazito ili kuhakikisha Simba dume anaibuka kidedea katika mpambano huo.

“tunapigana ili kuhakikisha songea  wanapatikana wapiganaji wengi wa ngumi kwa kuwa mchezo wa ngumi ni mchezo ambao unashika kasi  duniani kwa sasa hivyo itasadia vijana wengi kupata ajira.

Pia musa omari alisema siku ya sikuu ya noeli mwenzi huu anatarajia kupanda ulingoni kuvaana na Kosmas cheka pambano ambalo litapigwa songea mjini.


Chapisha Maoni