Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





Soka la Tanzania kwa miaka ya hivi karibuni limeonekana kukosa mwelekeo  baada ya timu ya taifa kufanya vibaya pamoja na vilabu katika mashindano mali mbali suala ambalo wadau na wachambuzi wengi wa soka ndani na nje ya Tanzania wamekuwa wakilizungumzia sana.

Mara nyingi viongozi wa vilabu bila kusahau Tff wanaraumiwa sana na mashabiki pamoja na wadau wa soka hapa nchini kwa kuendesha mpira kisiasa badala ya kuendesha  kisayansi kama ilivyo kwa nchi za wenzetu  hali ambayo imepelekea vilabu vyetu na timu ya taifa kufanya vibaya hasa kwa kipindi cha mika 15 ya hivi karibuni.

Lakini ukweli ni kwamba sio viongozi peke yao ndio wametufikisha hapa bali ni kukosekana kwa uzalendo toka  kwa Viongozi,wanachama pamoja na wachezaji ambao wameshindwa  kuweka maslai ya taifa mbele na Badala yake wametanguliza maslai yao na kulifanya soka la Tanzania kuendelea kubaki kuwa ni kichwa cha mwendawazimu,Tusilaumiane au kunyosheana vidole wakati tunajenga nyumba moja.


Kazi ya viongozi ni kuongoza,kazi ya wachezaji ni kucheza mpira na kazi ya wanachama ni kuchangia timu kwa hali na mali lakini inanvyoonekana kuwa  viongozi wanaingilia kazi ya wachezaji au wachezaji kuingilia kazi ya wanchana tayari linakuwa ni Tatizo na mwisho wa siku lazima itokee migogoro ambayo itapelekea timu kuyumba.
Kwa mara ya mwisho Tanzania kushiriki michuano ya mataifa huru ya Afrika ilikuwa ni mwaka 1980 inchini Nigeria ni takribani miaka 34 imepita sawa na umri wa mtu mzima,hii ni aibu kubwa kwa taifa kama la Tanzania ambalo watu wake wanapenda sana michezo.

Ili kuendeleza mpira wa Tanzania  watu wote bila kujali wazee au vijana lazima watambue kuwa maendeleo ya mpira wa nchi ya hii yapo mikononi mwao na sio mikononi mwa wachache,kama nchi itajitambua tunaamini viwanja vitajengwa,shule za michezo zitajengwa pia watu wenye taaluma ya mpira ndio watakabidhiwa  nyazifa zote zinazohusu mpira wa miguu,tofauti na ilivyo hivi sasa.



Chapisha Maoni