Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.


Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amesema  anakiogopa kichapo cha mabao 5-1 dhidi ya timu yake kilichotokea wakati wa mechi kati ya Liverpool na Arsenal msimu uliopita
Kocha wa kilabu ya Arsenal Arsene Wenger amekiri kwamba anaogopa kichapo cha 5-1 alichokipata wakati timu yake ilipochuana na Liverpool msimu uliopita, lakini akaongeza kuwa hatarajii kichapo kama hicho wakati timu hizo mbili zitakapokutana siku ya jumapili.

Arsenal ilikuwa imefungwa mabao 4-0 kufikia dakika ya 20 wakati wa mechi hiyo iliochezwa Anfield huku Liverpool ikiongozwa na mshambuliaji hatari ambaye ameihama kilabu hiyo Luis Suarez.Mechi hiyo ilikamilika ikiwa 5-1 dhidi ya Arsenal.
Lakini meneja huyo wa Arsenal anaamini mengi yamebadilika katika kipindi cha miezi 10,ikiwemo kuondoka kwa Suarez na jeraha la mshambuliaji Daniel Sturridge na mafanikio yake ya kumsajili Alexis Sanchez kutoka Barcelona mbele ya Breanda Rodgers.
Walikuwa wazuri sana katika safu ya mashambulizi,lakini msimu huu wamefunga mabao 19 pekee,hawana tena moto wa kufunga mabao waliokuwa nao.
Walianza kwa mori siku hiyo na sisi tulishindwa kujibu mashambulizi yao.
Kila mechi unayoshindwa inakua kovu katika moyo milele.Lakini tuna kumbukumbu nzuri katika uwanja wa liverpool.
Tulishinda mechi nyingi sana katika uwanja huo,lakini utakumbuka kwamba juma moja baadaye tuliweza kuishinda timu hiyo hiyo tulipocheza nayo nyumbani katika kombe la FA.'
 http://www.bbc.co.uk





Chapisha Maoni