Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.






Na Alex Mapunda,Iringa
Baada ya Polisi kusimamisha mkutano  mkuu wa Lipuli Jumapili iliyopita kwa madai kuwa viongozi wa timu hiyo hawakufuata taratibu, mkutano huo sasa umepangwa kufanyika kesho kutwa  wikendi hii katika ukumbe wa veta mkoani hapa.

Akizungumza na JELAMBA VIWANJANI katibu Msaidizi wa Lipuli Ronjino Malambo alisema kuwa Polisi waliwashauri kuhairisha mkutano huo kwa kuwa hawakufuata taratibu za kiusalama ili kuepuka madhara endapo zingetokea vurugu zozote katika mkutano huo.

“wote viongozi na wanachama ambao tulifika  kwa moyo mmoja na sasa tunafuata taratibu na mkutano huo utafanyika saa nne Asubuhi siku ya jumapili kama ambavyo tulipanga hapo awali”alisema Malambo. 

Akielezea mkutano huo mwenyekiti wa Lipuli AbuuMajeki alisema lengo kubwa na mkutano huo ni kuzungumzia matatizo ya Lipuli kushindwa kupanda daraja pia kumtatufa aliyesababisha timu hiyo isipande ligi kuu.

“Kutokana na wanachama kudai mara kwa mara mkutano mkuu wa Lipuli ili kujadili nani mchawi wa timu mimi nimeamua mkutano ufanyike siku ya Jumapili japo kuwa tarehe rasmi ya mkutano bado haijafika”

“Namegiza katibu wangu kuitisha kamati ya utendaji ili kujadili kuhusu mkutano huo lakini suala la kufanya mkutano jumapili mimi nimeshatanga mkutano lazima ufanyike siku ya Jumapili,alisema Majeki.

Majeki aliongeza kuwa wanachama wote wenye kadi na wasiokuwa na kadi wajitokeze kwa wingi katika uwanja wa Samora ili kusikiliza kitakachotokea siku hiyo ambapo kama itabainika Abuu Changawa ni chanzo cha Lipuli kufanya vibaya atatangaza kujiuzulu na kama sio yeye basi hatua kali zitachukuliwa kwa wale wote watakaobainika kuiujumu Lipuli.
 


Chapisha Maoni